ZAIDI ya Sh Bilioni 20 zimekusanywa kutoka kwa mashirika 40 yasiyo ya kiserikali pamoja na taasisi mbalimbali za serikali kwa ajili ya kusaidia katika kampeni za kupambana dhidi ya Virusi vya Ukimwi na Ukimwi ambapo tayari Mamilioni ya watanzania wamekwisha nufaika nazo.

Fedha hizo zimekusanywa kampuni ya Kuchimba dhahabu ya Geita (GGM) kupitia changamoto ya kupanda Mlima Kilimanjaro, ijulikanayo kama “Kili Challenge” tangu mwaka 2001 ilipoanzishwa ,mwaka huu ukiwa mwaka wa 17 ikishirikisha washiriki 70 watakao shiriki kupanda Mlima huku wengine wakizunguka mlima huo kwa kutumia Baiskeli .

Akizungumza wakati wa Hafla ya kuwaaga washiriki wa Programu ya Kili Challenge 20018 iliyofanyika katika lango la kupanda Mlima Kilimanjaro la Machame ,Makamu wa Rais wa GGM, Simon Shayo amesema Progaramu hiyo imepanua wigo wa kusaidia Taasisi zinazojikita kuhudumia wachimbaji wadogo wadogo pamoja na maeneo ya wavuvi ambako tafiti zinaonyesha wako kwenye mazingira hatarishi ya kuambukizwa VVU.

“Kila siku na kila mwaka ,tukio hili la hisani linaendelea kuwa na matokeo makubwa kwa jamii inayotuzunguka ,ninayo furaha leo kutagaza kwamba kupitia Kili Challenge tumeweza kuchangisha zaidi ya Bilioni 20 .”alisema Shayo.

Alisema fedha hizo zimekusanywa kutoka katika Mashirika 40 yasiyo ya kiserikali (N.G.O,S) pamoja na taasisi mbalimbali za serikali kupitia Tume ya taifa ya kudhibiti Ukimwi (TACAIDS) ambapo watanzania zaidi ya Milioni moja wamenufaika nayo.
 Mgeni Rasmi katika tukio hilo, Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu,Kazi,Vijana na Ajira ,Anthony Mavunde akikabidhi Bendera kwa washiriki wa changamoto hiyo kwa njia ya kuzunguka mlima Kilimanjaro kwa kutumia Baiskeli.
Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu,Kazi,Vijana na Ajira ,Anthony Mavundeakijaribu kuendesha Baiskeli kuashiria uzinduzi wa Changamoto ya kuzunguka Mlima Kilimanjaro kwa kutumia Baikeli.
 Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu,Kazi,Vijana na Ajira ,Anthony Mavundeakishirikia zoezi la Kupanda Mlima Kilimanjaro kuashiria mwanzo wa safari ya wapandaji 40 wanashiriki zoezi hilo. 
 Kamanda wa Polisi mkoa wa Kilimanjaro,Hamis Issah ni miongoni mwa washiriki walioanzisha safari hiyo. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...