Na Stella Kalinga, Simiyu
Serikali Mkoani Simiyu imeitaka jamii kushiriki kikamilifu katika suala la kupinga mimba za utotoni ili kukabiliana na ongezeko la mimba lililofikia 195  kwa wanafunzi wa Shule za msingi na Sekondari katika kipindi cha miaka mitatu  mkoani humo.

 Wito  huo umetolewa na Mkuu wa Wilaya ya Itilima, Mhe.  Benson Kilangi aliyemwakilisha Mkuu wa Mkoa  wa Simiyu, mhe. Anthony Mtaka katika Maadhimisho ya Siku ya Mtoto Afrika, yaliyofanyika Kimkoa katika Viwanja vya Shule ya Msingi Nanga B wilayani humo na kuhudhuriwa na wananchi na wadau wa maendeleo lengo likiwa ni kuikumbusha jamii haki za Mtoto.


Kilangi amesema Serikali haitawafumbia macho wale wote watakaowapa mimba wanafunzi hivyo akawataka wananchi kuungana na Serikali katika kulaani na kufichua wale wote wanaojihusisha na suala hilo ambalo linasababisha watoto wa kike kukatisha masomo yao.

“ Mpaka kufikia  mwaka 2016/2017 watoto 195 kati yao 25  wa shule za msingi na sekondari 170 wamepata mimba ndani ya mkoa wetu, hili ni tatizo na sisi hatutamfumbia macho wala kumlea mtu yeyote atakayempa mimba mtoto wa shule, niwaombe wananchi wote muungane na Serikali kulaani kwa nguvu zote mimba kwa watoto wetu wa kike” alisisitiza Kilangi
 Wanafunzi  wa shule za Msingi za kata ya Chinamili wilayani Itilima Mkoani Simiyu wakipita na mabango yenye jumbe mbalimbali mbele ya mgeni rasmi katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika Kimkoa yaliyofanyika katika Viwanja vya shule ya msingi Nanga B wilayani humo. 
 Mkuu wa Wilaya ya Itilima, Mhe.  Benson Kilangi (wa tatu kulia) na viongozi wengine wakipokea maandamano ya watoto(Kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu) katika maadhimisho ya Mtoto wa Afrika yaliyofanyika kimkoa wilayani Itilima katika viwanja vya Shule ya Msingi Nanga B.
 Kwaya ya wanafunzi wa Shule ya Msingi Senani wilaya ya Itilima mkoani Simiyu wakitoa burudani ya wimbo katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika yaliyofanyika kimkoa katika viwanja vya Shule ya Msingi Nanga B wilayani humo.
 Mtoto Luhangija Maduhu kutoka Shule ya Msingi Nanga B wilayani Itilima akisoma risala mbele ya Mkuu wa Wilaya  hiyo, Mhe. Benson Kilangi (ambaye alimwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka )kwa niaba ya watoto wa Mkoa wa Simiyu, katika Maadhimisho ya Siku ya Mtoto wa Afrika yaliyofanyika kimkoa wilayani Itilima katika viwanja vya Shule ya Nanga B. 
Mkurugenzi Mtendaji wa  Halmashauri ya Wilaya ya Itilima mkoani Simiyu, Bw. Mariano Mwanyigu akitoa taarifa fupi kuhusu Maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika, ambayo yamefanyika kimkoa wilayani humo katika Viwanja vya Shule ya Msingi Nanga B. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...