Na Karama Kenyunko, Blogu ya jamii
KATIKA kuadhimisha miaka kumi ya M-PESA kampuni ya simu ya mkononi Vodacom Tanzania imesherekea hafla hiyo ya kwa kutoa futari kwa wateja wake na kuwahamasisha waendelee kutumia huduma hiyo ya haraka na uaminifu.

Akizungumza wakati wa hafla hiyo, iliyofanyika Mlimani City jijini Dae es Salaam, Mkurugenzi Msaidizi wa Utawala, Wizara ya Ujenzi Uchukuzi na Mawasiliano  Mary Majula, amesema serikali itaendelea kuwa bega kwa bega, kusimamia fedha za wateja na kuhakikisha hakuna wizi au utapeli kupitia mitandaoni.

Pia amewapongeza Vodacom kwa kuwa kinara wa wateja wengi wanaofanya miamala ambapo kwa mwezi Machi tu wateja zaidi ya milioni nane walifanya miamala ya kifedha.

Nae Mkurugenzi wa Vodacom, Ian Ferrao amesema sherehe hizo zitaendelea kufanyika katika mikoa tofauti nchi nzima kwa kuwa huduma M-PESA ndiyo inayoongoza nchini Tanzania ikiwa imekamata asilimia 42 ya soko, watumiaji hai zaidi ya milioni 8.2.
  Mkurugenzi Msaidizi wa Utawala, Wizara ya Ujenzi Uchukuzi na Mawasiliano  Mary Majula ( wa sita kushoto) akiiongoza meza kuu kushuhudia magari mawili kati ya 10 yatakayoshindaniwa na wateja wa M-Pesa  yaliyotolewa wakati wa hafla ya kutimiza miaka kumi ya M-Pesa iliyofanyika jana Jijini Dsm. Wengine pichani ni Kaimu Mkurugenzi wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Dkt.Raymond Mfungahema (wa tano kushoto), Mkurugenzi  Mtendaji wa Vodacom Tanzania, Ian Ferrao, Mkurugenzi wa kitengo cha M-pesa Ashutosh Tiwary na Mkurugenzi wa Mifumo ya malipo ya Kitaifa wa Benki Kuu Tanzania (BoT) Benard Dodi.
 Mgeni rasmi katika sherehe ya miaka 10 ya M-Pesa, Mkurugenzi Msaidizi wa Utawala, Wizara ya Ujenzi Uchukuzi na Mawasiliano  Mary Majula (wa kwanza kushoto),  Mkurugenzi wa Mifumo ya malipo ya Kitaifa wa Benki Kuu Tanzania (BoT) Benard Dodi, Kaimu Mkurugenzi wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Dkt.Raymond Mfungahema  na Mkurugenzi  Mtendaji wa Vodacom Tanzania, Ian Ferrao,  wakifuatilia moja ya burudani wakati wa sherehe ya kusherehekea mika 10 ya M-PESA iliyofanyika katika Ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam.
 Mkurugenzi Msaidizi wa Utawala, Wizara ya Ujenzi Uchukuzi na Mawasiliano  Mary Majula (kulia)   akimsikiliza Mkurugenzi wa Mawasiliano na Uhusiano wa Vodacom Tanzania Plc, Rosalyn Mworia (katikati)  wakati wa hafla ya kusherekea miaka 10 ya M-pesa iliyofanyika  katika Ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Ian Ferrao.
 Mkurugenzi wa Mawasiliano na Uhusiano wa Vodacom Tanzania Plc, Rosalyn Mworia  akimsikiliza mkurugenzi Msaidizi wa Utawala, Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano  Mary Majula  wakati wa  hafla ya kusherekea miaka 10 ya M-pesa  iliyofanyika  katika Ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam.
 Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Tanzania, Ian Ferrao (kulia) akisalimiana na balozi wa Afrika Kusini nchini Tanzania, Thomsanga Msekelu  wakati wa Sherehe ya Kusherehekea miaka 10 ya M-pesa iliyofanyika Mlimani City jijini Dar es Salaam jana.
 Moja ya magari mawili kati ya 10 yatakayoshindaniwa na wateja wa M-Pesa  yakiwa katika ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam, mara baada ya kuzinduliwa  wakati wa sherehe kusherehekea miaka 10 ya M-pesa .Kulia ni Mkuu wa kitengo cha Maendeleo ya Biashara wa M-Pesa, Polycarp Ndekana  na mshereheshaji Taji Liundi.
 Mkurugenzi wa Mawasiliano na Uhusiano wa Vodacom Tanzania Plc, Rosalyn Mworia (kulia) Mkurugenzi wa kitengo cha M-pesa Ashutosh Tiwary  (katikati) na Mkuu wa kitengo cha Mwendelezo  wa Biashara ya M-Pesa, Polycarp Ndekana wakiangalia moja ya gari kati ya 10 yatakayoshindaniwa na wateja wa M-pesa  wakati wa sherehe ya kusherehekea miaka k10 ya M-pesa  iliyofanyika  katika Ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam.


KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...