Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akimkaribisha Mjumbe Maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa katika Maziwa Makuu Mhe. Said Djinnit alipomtembelea Wizarani terehe 13 Juni 2018, Dar es Salaam. Anayeshuhudia kushoto ni Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa, Bw. Alvaro Rodriguez.

Mjumbe huyo alifika Wizarani kwa lengo la kuzungumzia hali ya usalama na amani katika nchi za Maziwa Makuu.Aidha, mjumbe huyo alimuomba Mhe. Waziri kufikisha shukrani zake kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. John Pombe Magufuli kwa mchango mkubwa wa Tanzania katika kusaidia kutunza amani ya nchi za Maziwa Makuu.

 Mhe. Waziri Mahiga akiwa katika mazungumzo na mgeni wake Mhe.Djinnit.
Mkutano ukiendelea, wanaoshuhudia ni Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Afrika Bw. Salvatory Mbilinyi(wa kwanza kulia kwa Waziri), Bw. Ally Ubwa Afisa Mambo ya Nje na Bw. Magabilo Murobi Katibu wa Waziri na kushoto ni Ujumbe wa Mhe. Djinnit alioongozana nao.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...