Meneja wa Mawasiliano wa Chuo Kikuu Mzumbe Rosada Fredrick akizungumza na waandishi kufanya udahili katika maonesho ya Vyuo Vikuu.
Wanfunzi wakipata maelezo katika banda la Chuo Kikuu Mzumbe.
CHUO Kikuu Mzumbe kimesema kuwa katika maonesho vyuo vikuu katika viwanja vya Mnazi mmoja wanadahili moja kwa moja kwa njia kieletroniki kwa wale wanaotaka kujiunga na chuo hicho.
Akizungumza katika maonesho hayo Meneja Mawasiliano wa Chuo hicho Silvia Lupembe amesema katika maonesho hayo watanzania watumie fursa ya kupata taarifa za chuo hicho na wataotaka kujiunga watafanya udahili kwa kupata muongozo kwa watumishi waliopo katika maonesho.
Amesema Chuo Kikuu Mzumbe kinahistoria katika utoaji wa elimu bora hivyo ni fursa katika maonesho kwa wananchi kutembelea na kupata taarifa za chuo.
Lupembe amesema wakati kuwa dirisha liko wazi kwa waombaji kuomba kwa njia ya kieletroniki.
"Tunajivunia katika utoaji wa elimu bora kwa wanafunzi hivyo ni fursa kwao vijana kujiunga na chuo hicho"amesena.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...