Na Karama Kenyunko, Globu ya jamii
MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Morogoro, imezuia watuhumiwa wanaoachiwa kwa kifungu ambacho kinaruhusu wao kukamata, kukamatiwa ndani ya viunga vya mahakama hiyo.

Hayo yameelezwa leo mkoani hapa na Hakimu Mkazi Mwandamizi Mfawidhi wa Mkoa wa Morogoro Elizabethi Nyembele wakati wa ziara ya waandishi wa habari za mahakamani walipofika katika Mahakama hiyo.

Waandishi hao wapo katika mafunzo ya siku tano yambayo yameandaliwa na Mahakama ya Tanzania kwa kushirikiana na Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto chini ya ufadhili wa Benki ya Dunia.Mafunzo hayo yameahirikisha waandishi 30 wa vyombo mbalimbali nchini.

Amesema, wamezungumza na Polisi wasiwakamate watuhumiwa pindi wanapokuwa wameachiwa ndani ya viwanja vya Mahakama kwani ni fedhea.

" Tumezungumza na Polisi wasifanye hivyo, kwa sababu mara nyingine mshtakiwa anakamamatwa hata mbele ya hakimu bila kujali wapo katika eneo gani,

" Mtuhumiwa anakufuata anakwambia mheshimiwa naomba nilinde wanataka kunikamata kitendo ambacho si kizuri na hakileti picha," amesema Hakimu Nyembele

Ameongeza kuwa, hakimu anapoifuta kesi huku akijua inahitilafu kisheria anamueleza mtuhumiwa kuwa anaweza kufunguliwa kesi nyingine.Wengine ni waelewa unamuachia pale pale anaingia mikono ni mwa polisi bila kukimbia
Hakimu Mkazi  Mwandamizi  Mfawidhi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Morogoro Elizabeth Nyembele akizungumza na waandishi wa habari leo wakati walipotembelea katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Morogoro kwenye moja ya ziara za kimafunzo kwa Waandishi wa habari za mahakama mkoani Morogoro
Hakimu Mkazi Mwandamizi Mfawidhi Mahakama ya Hakimu Mkazi Morogoro  Elizabeth Nyembele akizungumza na wananchi waliokuwa wakisubiri kuanza kwa mashauri yao kwenye Mahakama ya Hakimu Mkazi Morogoro katika ziara ya kimafunzo kwa waandishi wa habari  mkoani Morogoro.  (PICHA NA JOHN BUKUKU-FULLSHANGWE-MOROGORO)
Hakimu Mkazi Mwandamizi Mfawidhi Mahakama ya Hakimu Mkazi Morogoro  Elizabeth Nyembele akionyesha waandishi wa habari nembo ya iliyopo kwenye Mahakama ya Hakimu Mkazi Morogoro.
Baadhi ya waandishi wa habari wakisikiliza maelezo ya Hakimu Mkazi Mwandamizi Mfawidhi Mahakama ya Hakimu Mkazi Morogoro Mhe. Elizabeth Nyembele hayupo kwenye picha.
Mtendaji wa Mahakama mkoa wa Morogoro Nestory Mjunangoma akizungumza na waandishi wa habari wakati ziara ya kimafunzo kwa waandishi wa habari mkoani Morogoro.
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...