Mkuu wa wilaya ya Monduli Mhe.Idd Hassan Kimanta ametembelea waathirika wa janga la moto huko katika kijiji cha Irerendeni kata ya Engaruka akiwa amefuatana na baadhi ya wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama na Mbunge wa Jimbo la Monduli Mhe.Julias Kalanga 
Kwenye ziara hiyo viongozi hao walijionea adha iliyokumba wafanyabishara hao kwa kuunguliwa na vibanda vyao vya maduka  kwa moto ulioanza tarehe 17.07.2018 saa saba usiku na kudumu kwa saa tano na kuleta athari kubwa na kifo kwa mfanyabiashara mmoja aliyejulikana ka kwa jina la Siriel massawe ambaye umauti ulimkuta baada kuzidiwa na moto mkubwa ndani. 
Jumla ya maduka saba yaliteketea kwa moto na Mkuu wa wilaya aliwapa pole sana waathirika na kuwataka kuwa watulivu wakati vyombo vya ulinzi vikifanya uchunguzi.  
Pia kupitia Halmashauri ya Wilaya ya Monduli imeahidi kutoa mkono wa pole Tsh.200.000/= kwa kila mfanyabiashara na kuwalipia madeni ya Mikopo yao waliokopa kwenye taasisi za kifedha baada uhakiki mikopo yao.  
  Mkuu wa wilaya ya Monduli Mhe. Idd Hassan Kimanta (mwenye fimbo) akikagua madhara ya moto uliotokea katika kijiji cha Irerendeni kata ya Engaruka akiwa amefuatana na baadhi ya wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama na Mbunge wa Jimbo la Monduli Mhe.Julias Kalanga 
 Sehemu ya eneo likionesha madhara ya moto uliotokea katika kijiji cha Irerendeni kata ya Engaruka akiwa amefuatana na baadhi ya wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama na Mbunge wa Jimbo la Monduli Mhe.Julias Kalanga 
 Madhara ya moto huo
Mkuu wa wilaya ya Monduli Mhe.Idd Hassan Kimanta akitoa maelekezo na kuwapa pole kwa waathirika wa  madhara ya moto uliotokea katika kijiji cha Irerendeni kata ya Engaruka akiwa amefuatana na baadhi ya wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama na Mbunge wa Jimbo la Monduli Mhe.Julias Kalanga 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...