Na Chalila Kibuda,Globu ya Jamii.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk.John Pombe Magufuli amesema kuwa ukombozi kwa ajili ya Uhuru ulishapita sasa ni ukombozi wa maendeleo ya Kiuchumi.

Rais Dk. Magufuli ameyasema hayo leo wakati wa kuweka Jiwe la Msingi la Ujenzi wa Chuo cha Mwalimu Julius Nyerere Kinachojengwa Kwa Mufipa , Kibaha mkoani Pwani, amesema kuwa chuo hicho kikamilika kitasaidia kutoa elimu kwa makada na viongozi.

Chuo hicho kinajengwa nchini mahsusi kwa ajili vyama sita vilivyopigania ukombozi wa Afrika kwa kupata msaada na China.Vyama hivyo vilivyopigania ukombozi wa Afrika ni ZANU PF ya Zimbabwe, SWAPO - Namibia, AMPLA- Angola, ANC- Afrika Kusini pamoja na FRELIMO- Msumbiji

Katika uzinduzi huo makatibu wa Wakuu wa Vyama vya Ukombozi walihudhuria wakiongozwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wa Chama cha CPC cha nchini China.Amesema kuwa CPC imekuwa mstari mbele lakini wamekwenda mbele kiuchumi.

Amesema kuwa katika chuo hicho watazaliwa wakina Nyerere wapya na Nelson Mandela , Agustino Netho na Samora Machel.Rais Magufuli amewagiza Makatibu wa Wakuu wa Vyama hivyo kufanya maandalizi mapema ya mitaala pamoja na wakufunzi ili Chuo kikamilika kila kitu kimekamilika.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na mgeni wake Waziri wa uhusiano wa Kimataifa wa Chama cha Kikomunisti cha China (CPC) Song Tao wanne kutoka kushoto pamoja na Makatibu wa vyama vya, CCM, ANC, SWAPO, ZANU-PF, MPLA, FRELIMO, wakiweka mchanga kama ishara ya uwekaji wa Jiwe la msingi Ujenzi wa Chuo cha Mwalimu Julius Nyerere kinachojengwa katika eneo la Kibaha kwa mfipa mkoani Pwani.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika picha na mgeni wake Waziri wa uhusiano wa Kimataifa wa Chama cha Kikomunisti cha China (CPC) Song Tao wanne kutoka kushoto waliokaa, viongozi wa vyama vya ANC, SWAPO,ZANU-PF, MPLA, FRELIMO pamoja na viongozi mbalimbali wa Chama cha Mapinduzi CCM mara baada ya kuweka jiwe la msingi ujenzi wa Chuo cha Uongozi cha Mwalimu Julius Nyerere kinachojengwa katika eneo la Kibaha kwa mfipa mkoani Pwani. Chuo hicho kinajengwa na Chama cha Kikomunisti cha China (CPC) kwa gharama ya Shilingi Bilioni mia moja(100). 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza jambo na mgeni wake Waziri wa uhusiano wa Kimataifa wa Chama cha Kikomunisti cha China (CPC) Song Tao kabla ya tukio la uwekaji jiwe la msingi ujenzi wa Chuo cha Uongozi cha Mwalimu Julius Nyerere kinachojengwa katika eneo la Kibaha kwa mfipa mkoani Pwani.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Dkt. John Pombe Magufuli akipiga ngoma pamoja Sophia Shaningwa Katibu wa Chama cha SWAPO kutoka nchini Namibia huku Waziri wa uhusiano wa Kimataifa wa Chama cha Kikomunisti cha China (CPC) Song Tao akipiga makofi mara baada ya uwekaji wa jiwe la msingi ujenzi wa Chuo cha Uongozi cha Mwalimu Julius Nyerere kinachojengwa katika eneo la Kibaha kwa mfipa mkoani Pwani.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Dkt. John Pombe Magufuli akiangalia mfano wa moja ya majengo ya chuo hicho kitakapo kamilika kujengwa. 
PICHA NA IKULU
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...