Na said Mwishehe, Globu ya jamii 

SEKRETARIETI ya Maadili ya Viongozi wa Umma imeamua kuwanoa viongozi wanawake wa ngazi mbalimbali wakiwamo madiwani na wakuu wa Idara katika manispaa za Mkoa wa Dar es Salaam kwa lengo la kuwajengea uelewa kuhusu maadili ya viongozi wa umma. 

Akizungumza leo jijini Dar es Salaam wakati anafungua semina ya mafunzo hayo Kamishina wa Sekratarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Harold Nsekela amesema yatatoa fursa kwa viongozi hao kufahamu sekretarieti kuanzia majukumu, kazi na wajibu walionao katika usimamizi wa maadili.

Amefafanua sababu za kutolewa kwa mafunzo yametokana na utafiti uliofanywa mwaka 2015 kupitia taaaisi yao ya Kukuza uelewa wa wananchi kuhusu majukumu na kazi zinazotekelezwa na sekretarieti hiyo. "katika utafiti huo iliyokuwa unapoona ushiriki wa utoaji wa taarifa uliofanywa na makundi mbalimbali katika jamii kuhusu ukiukwaji wa maadili miongoni mwa viongozi wa umma. 

"Matokeo yalionesha ni asilimia moja tu ya wanawake kwenye vijiji na mitaa walishiriki kutoa taarifa za ukiukwaji wa maadili, "amesema. 

Amesema hali hiyo ililazimu Sekretarieti ya maadili ya viongozi wa umma kuandaa mafunzo hayo katika mikoa yote inayotekelezwa mradi huo ambayo ni Mtwara, Morogoro, Iringa na Dodoma. "Lengo la mafunzo haya ni kuwajengea uelewa viongozi wanawake katika mamlaka za Serikali za mitaa kuhusu maadili ya viongozi wa umma.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...