SERIKALI ya Tanzania imeomba wadau wa maendeleo na taasisi mbalimbali zikiwemo za Umoja wa Mataifa kuendelea kufanyakazi nayo kuhakikisha kwamba ajenda ya kimataifa ya maendeleo endelevu ifikapo mwaka 2030 inaendelea kutekelezwa nchini.
Hayo yalisemwa katika kikao cha kupewa taarifa ya utekelezaji wa malengo hayo na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Dk Augustine Mahiga.
Aidha alisema serikali imetengeneza mikakati kadhaa ya kuwezesha kutekelezwa kwa malengo hayo ya dunia.
Alisema wakati Tanzania imekaza nia ya kuwa na uchumi wa kati unaotegemea viwanda suala linalosisitizwa katika SDG 9 ni muhimu na kwamba serikali ya Tanzania inataka kuendeleza ushirikiano huo ili malengo ya dunia yafikiwe pia nchini Tanzania.
Alisema Tanzania chini ya uongozi wa Rais John Magufuli inaendelea kutekeleza mpango wa maendeleo endelevu wa Umoja wa Mataifa (SDGs) wenye lengo la kufikia ustawi kwa kila mkazi wa dunia hii.
Ili kutekeleza malengo hayo, mpango wa maendeleo wa miaka mitano umeingiza malengo ya SDGs.
“Kama nchi tangu tumeanza kutekeleza SDG kwenye  mwaka 2016, tumechambua na kuingiza vipengele vya SDGs kwenye mipango mbalimbali ya kitaifa ikiwamo mpango wa pili wa maendeleo wa miaka mitano 2016/17-2020/21 (FYDP II) na mpango wa tatu wa kukuza uchumi wa Zanzibar na kupunguza umaskini (MKUZA III)” alisema.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Dk. Augustine Mahiga akitoa neno la ufunguzi wakati wa kikao cha kupewa taarifa ya utekelezaji wa maendeleo endelevu kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Fedha na Mipango, Dk. Philip Mpango akizungumza kwenye kikao cha kupewa taarifa ya utekelezaji wa maendeleo endelevu kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Profesa Adolf Mkenda akitoa neno la ukaribisho wakati wa kikao cha kupewa taarifa ya utekelezaji wa maendeleo endelevu kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam.
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez akitoa maelezo mafupi kuhusu mkutano wa mashauriano baina ya Serikali ya Tanzania na mashirika ya Umoja wa Mataifa wakati wa kikao cha kupewa taarifa ya utekelezaji wa maendeleo endelevu kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam. Kulia ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Profesa Adolf Mkenda
Balozi wa Norway nchini Tanzania, Hanne-Marie Kaarstad akitoa maoni wakati wa kikao cha kupewa taarifa ya utekelezaji wa maendeleo endelevu kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam.
Balozi wa Malawi nchini Tanzania, Hawa Ndilowe akizungumza wakati wa kikao cha kupewa taarifa ya utekelezaji wa maendeleo endelevu kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam.
Kaimu Mkuu wa Ofisi za Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) nchini, Faith Shayo akibadilishana mawazo na mmoja wa wadau wa maendeleo wakati wa kikao cha kupewa taarifa ya utekelezaji wa maendeleo endelevu kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam
 Baadhi ya wadau wa maendeleo, viongozi mbalimbali wa serikali pamoja na Waheshimiwa mabalozi wanaowakilisha nchi zao hapa nchini walioshiriki kikao cha kupewa taarifa ya utekelezaji wa maendeleo endelevu kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam
Picha ya pamoja ya viongozi wa serikali, wadau wa maendeleo kutoka mashirika mbalimbali na mabalozi wanaowakilisha nchi zao hapa nchini mara baada ya kumalizika kwa kikao cha kupewa taarifa ya utekelezaji wa maendeleo endelevu kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam.


KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...