WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewataka wanasiasa wakiwemo mawaziri na wabunge wawahamishe Watanzania kuendeleza utamaduni wao.
Ametoa wito huo leo (Jumatano, Julai 18, 2018) wakati akizungumza na wazee na wananchi wa Makunduchi mara baada ya kushuhudia maadhimisho ya sikukuu ya Mwaka-Kogwa yaliyofanyika Makunduchi, wilaya ya Kusini, mkoa wa Kusini Unguja, Zanzibar.
“Mawaziri wote, tuna dhamana ya kuwahamasisha Watanzania waendeleze utamaduni ili uwe ni jambo hai. Wabunge na wawakilishi tukiwa kwenye majukwaa, tusisitize Watanzania waendeleze utamaduni,” amesema.
Amesema Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (SMT) pamoja na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) zinasimamia uwepo wa utamaduni na zenyewe zinaongozwa na Ilani ya Chama cha Mapinduzi ambayo imelenga kuihamasisha jamii kuuenzi, kuulinda na kuudumisha utamaduni wa Mzanzibari na kushiriki katika uandaaji wa matamasha 50 ya utamaduni.
“Lazima utamaduni uendelezwe ndani na nje ya nchi na ni lazima tufanye jitihada tuwarithishe watoto utamaduni wetu. Kwa mfano, hapa Zanzibar mnalo tamasha la ZIFF, lile ni la kimataifa, vyombo vya muziki ni vya kisasa. Ni vema sasa, tukaangalia uwezekano wa kuwa na tamasha la huku chini ambalo litatumia ala za muziki za asili,” alisema.
Akizungumzia sherehe za Mwaka Kogwa, Waziri Mkuu alisema hii ni mara yake ya kwanza tangu azaliwe kuona watu wakichapana viboko si kwa ugomvi wala chuki, bali wakiwa na furaha.
“Mwaka Kogwa ni utamaduni wetu, pande zote za visiwani na zimekuwa zikifanyika kila mwaka lakini hivi sasa ni Makunduchi peke yake ambao mmeweza kuendeleza utamaduni huu, wengine wameacha kuadhimisha sherehe hizi,” amesema.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akikata utepe kuhitimisha Sherehe za Mwakakogwa, eneo la Makunduchi Zanzibar Julai 18, 2018.
Waziri
Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza katika Sherehe za Mwakakongwa
zilizofanyika Makunduchi Zanzibar Julai 18, 2018. Kushoto ni Mkuu wa
Mkoa wa Kusini Unguja, Hassan Khatib Hassan. (Picha na Ofisi ya Waziri
Mkuu)
Sehemu ya umati wa watu waliohudhuria katika Sherehe za Mwakakogwa zilizofanyika Makunduchi Zanzibar Julai 18, 2018.
Waziri
Mkuu, Kassim Majaliwa akishiriki katika sala ya kumwombea Rais wa Awamu
ya Nne wa Zanzibar, Idris Abdul Wakil kwenye kaburi la Rais huyo enero
la Makunduchi, Zanzibar Julai 18, 2018. Wengine pichani kutoka kushoto
ni Waziri wa Ujenzi, Mawasiliano na Usafirishaji, Sira Ubwa Mwamboya,
Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja , Ayoub Mohammed Mahmoud na Mkuu
wa Mkoa wa Kusini Unguja, Hassan Khatib Hassan.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Mohammed Abdulwakil ambaye
ni Kaka wa Rais wa Awamu ya Nne wa Zanzibar, Idris Abdul Wakil
Wakati alipozulu kaburi la Rais huyo, eneo la Makunduchi, Zanzibar
Julai 18, 2018. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri
Mkuu, Kassim Majaliwa akivalishwa kofia na Mwenyekiti wa Kamati ya
Maandalizi ya Sherehe za Mwakakogwa, Mwalimu Makungu Mwita katika
sherehe za Mwakakogwa zilizofanyika Makunduchi Zanzibar Julai 18, 2018.
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...