Na Said Mwishehe, Globu ya jamii
VYAMA vilivyoshiriki kupigania ukombozi wa Bara la Afrika sasa vimetakiwa kuingia awamu ya pili ya ukombozi wa kiuchumi kwa ajili ya maendeleo ya Bara la Afrika huku vikitakiwa kukomesha rushwa, ufisadi na ubadhirifu.

Hayo yamesemwa leo jijini Dar es Salaam na Makamu wa Pili wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Balozi Seif Ali Idd wakati anafunga mkutano wa siku mbili uliohusisha vyama vilivyokuwa mstari wa mbele kupigania ukombozi Kusini mwa Bara la Afrika.

"Awamu ya kwanza ilikuwa ni kupigania uhuru kwa nchi za Afrika na sasa uhuru tunao, hivyo vyama hivyo vinatakiwa kuingia awamu ya pili ya ukombozi wa kiuchumi.

"Kuna kila sababu ya kujifunza kutoka China ambapo wameendesha mapinduzi ya kiuchumi na  kuwakomboa wananchi wake wapatao bilioni  mbili,"amesema.

Amefafanua kama si China mambo yangekuwa mabaya na kama ingekuwa inatolewa Kombe la Dunia kwa nchi ambayo imefanikiwa kujenga uchumi imara basi kombe lingekwenda China.

Balozi Idd amesema China imekuwa ikitoa msaada kwa nchi mbalimbali za Afrika ikiwamo Tanzania ambayo imekuwa ikinufaika na misaada ya nchi hiyo na miradi mbalimbali ambayo imeacha alama isiyofutika akitolea mfano reli ya TAZARA.

Amesema kwa upande wa Zanzibar kuna miradi mingi ya maendeleo imefanyika ikiwamo pia ujenzi wa kiwanda cha sukari , viwanja vya kisasa vya mpira.

Akifafanua zaidi kuhusu mkutano huo, amesema ni vema yale ambayo wamekubaliana yakatekelezwa kwa vitendo na si maneno matupu.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akiufunga mkutano wa Vyama vya Kisiasa Barani Afrika na Chama cha Kikoministi cha China ukiofanyika kwa siku mbili Jijini Dar es Salaam .
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Uhusiano wa Kimataifa kutoka Chama cha Kikoministi cha China (CPC)  Xu Lyuping akitoa salamu za Chama cha Kikoministi wakati wa kufungwa  kwa mkutano wa Vyama vya Kisiasa Barani Afrika na Chama cha Kikoministi cha China leo Jijini Dar es Salaam.
Katibu Mkuu wa Chama Kinachotawala Nchini Cape Vade Bwana Miguel Petro akitoa salamu za Chama hicho wakati wa kufungwa  kwa mkutano wa Vyama vya Kisiasa Barani Afrika na Chama cha Kikoministi cha China leo Jijini Dar es Salaam. Picha na – OMPR – ZNZ.


KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...