ZIARA ya Kamishina msaidizi (ulinzi) kutoka shirika la wakimbizi Duniani (UNHCR),Volker Turk imehitimishwa jijini Dar es salaam huku akihimiza kuwa kila mkimbizi ana haki ya kuamua aidha kurejea nchini kwake au la.

Turk amekuwa nchini kwa siku nne kuanzia Agosti 13 mpaka Agosti 16 Agosti 2018 ,Turk amehitimisha ziara yake kwa kukutana na wanahabari jijini Dar es salaam, katika ziara hiyo aliambatana na Mratibu wa tume Afrika Valentin Tapsob na Mratibu wa wakimbizi (kanda) kutoka Burundi bi. Catherine Wiesner.

Lengo la ziara hiyo ya Kamishina kutoka UNHCR ilikuwa ni kufanya majadiliano yaliyohusisha serikali na wadau kuhusu changamoto na masuluhisho kwa zaidi ya wakimbizi 34o,000 na wale wanaoomba hifadhi (asylum seekers) nchini.Imeelezwa kuwa idadi kubwa ya wakimbizi waliopo nchini wanatoka katika nchi za Burundi na Jamuhuri ya kidemokrasia ya Kongo ambapo asilimia 87 wanaishi katika kambi 3 zilizopo Mkoani Kigoma.

Kamishina Turk pia ametembelea kambi ya wakimbizi Nduta ambapo alishuhudia mchakato wa kuwarejesha makwao wakimbizi kutoka Burundi na hadi sasa zaidi ya wakimbizi 42,000 wamerejea nchini Burundi.

" Haki ya wakimbizi lazima iheshimiwe katika kuamua kurejea nchini mwao au la" amesema Turk na kuongeza kuwa maamuzi hayo yaangalie taarifa iliyotolewa bila kulazimishwa aidha arejee au la.Pia wawakilishi kutoka nchini Burundi wamekutana na Kamishina Turk na kueleza kuwa idadi ya wakimbizi imefikia 400,000 hadi kufikia Julai 31 mwaka huu.

Aidha imesemwa kuwa hali ya wakimbizi kutoka Burundi imekua chini zaidi duniani katika kupokea misaada ya kibinadamu, UNHCR na washirika wengine walipokea asilimia 12 ya dola milioni 391 za kimarekani pekee kwa mwaka 2018 na mwaka 2017 asilimia 21 ya misaada ilipokelewa kwa ajili ya wakimbizi kutoka Burundi.

Kutokana na hali hiyo Turk ameiomba jumuiya ya kimataifa kuangalia hali hiyo ya kusahaulika kwa wakimbizi katika kupatiwa misaada ya kibinaadamu.Katika ziara hiyo ambayo Kamishina Turk alikutana na mamlaka za serikali, wakuu wa balozi, wafadhili na wadau mbalimbali nchini ameaidiwa kuwa Tanzania itahakikisha maamuzi ya wakimbizi katika kurejea nchini kwao yataheshimiwa.
Kamishina msaidizi (ulinzi) kutoka shirika la wakimbizi Duniani (UNHCR),Volker Turk akizungumza mbele ya Waandishi wa Habari (hawapo pichani) jana jijini Dar kuhusiana na ziara yake ya siku nne,lengo ya ziara hiyo ilikuwa ni kufanya majadiliano yaliyohusisha serikali na wadau kuhusu changamoto na masuluhisho kwa zaidi ya wakimbizi 340,000 na wale wanaoomba hifadhi (asylum seekers) nchini.
Kamishina msaidizi (ulinzi) kutoka shirika la wakimbizi Duniani (UNHCR),Volker Turk akizungumza mbele ya Waandishi wa Habari jana jijini Dar kuhusiana na ziara yake ya siku nne,lengo ya ziara hiyo ilikuwa ni kufanya majadiliano yaliyohusisha serikali na wadau kuhusu changamoto na masuluhisho kwa zaidi ya wakimbizi 340,000 na wale wanaoomba hifadhi (asylum seekers) nchini.Pichani kushoto ni Mratibu wa tume ya Afrika Valentin Tapsob,Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia Wakimbizi Tanzania (UNHCR), Chansa Kapaya na kulia ni Mratibu wa wakimbizi (kanda) kutoka Burundi,Catherine Wiesner.
Baadhi ya Wanahabari wakimsikiliza Kamishina msaidizi (ulinzi) kutoka shirika la wakimbizi Duniani (UNHCR),Volker Turk alipokuwa akizungumza nao kuhusu ziara yake ya siku nne aliyoifanya nchini Tanzania

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...