Na Felix Mwagara, MOHA
WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola amewapa wiki moja Jeshi la Polisi Wilaya
Bunda, kuwakamata wanafunzi watoro, wazazi wa wanafunzi watoro pamoja na watu
waliowarubuni wanafunzi wa kike ambao wameacha shule wilayani humo.
Lugola ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Mwibara, wilayani Bunda, Mkoa wa Mara, alisema
inamsikitisha sana idadi kubwa ya wanafunzi wilayani humo wameacha masomo yao na
kurubuniwa wanaume ili waweze kuolewa huku Serikali ikitangaza elimu bure kuanzia shule za
msingi mpaka kidato cha nne.
Akizungumza na mamia wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika Uwanja wa mpira wa
miguu wa Busambara, Kijiji cha Busambara, Kata ya Kitengule, wilayani humo, Lugola alisema
kiwango cha wanafunzi kuacha masomo inatisha, hivyo serikali haiwezi kukaa kimya, lazima
kuhakikisha wanafunzi hao wanasoma ili waje kuwa viongozi wa nchi.
“Mkuu wa Polisi wa hapa Bunda, nawapa wiki moja, mtumie elimu zenu za upelelezi
mliofundishwa, wakamateni, wachunguzeni, wahojini ndugu, jamaa, majirani mtawawapata
wote wanaowarubuni watoto hawa, halafu mushughulike nao,” alisema Lugola.
Pia Lugola aliongeza kua, kuna sheria zinazoshughulika na wanafunzi watoro na pia zipo sheria
zinazoshughulika na wazazi wa wanafunzi watoro, pia zipo sheria zinazowashughulikia
wanaume wanaowarubuni wanafunzi, hivyo haiwezekani wanafunzi wa kidato cha tano wakatae
masomo, na wengi wao wanaokataa masomo ni wasichana.
Aidha, Lugola alisema ujenzi wa sekondari mbili za kidato cha tano na sita unaendelea ambapo
katika kata za Nansimo na Muramba katika Jimbo lake la Mwibara zitanaanza kuchukua
wanafunzi mwaka ujao watakao fanya mtihani wa kidato cha nne mwaka huu.
“Tunaendelea kuweka miundombinu katika shule hizo ili ziweze kuchukua wanafunzi wa kidato
cha tano katika maeneo haya na hatutarajii wanafunzi kukosa shule wamalizapo kidato cha nne,”
alisema Lugola.
Hata hivyo, Lugola pia aliwataka polisi nchini kuwakamata waendesha magari na bodaboda
ambao hawafuati sheria za barabarani ikiwemo baadhi ya bodaboda uvunja sheria kwa makusudi
kwa kupakia abiria wanne na kuendelea ambapo ni hatari kwa usalama wa dereva na abiria hao.
“Idadi kubwa ya polisi wanafanyakazi kwa umakini na uaminifu mkubwa, ila wachache sana
ndio wenye tabia hizo mbaya, nawataka askari hao wafuate sheria na pia kuendelea kuzikamata
kama ni magari au bodaboda au wananchi wowote ambao wanavunja sheria za nchi,” alisema
Lugola.
Waziri Lugola yupo katika ziara jimboni kwake kwa kutembelea miradi mbalimbali ya
maendeleo pamoja na kuwaunganisha wananchi kupitia Bonanza lake la michezo ya mpira wa
miguu ambalo linashirikisha kila kata wakitoa washindi mbalimbali ambao anawapa zawadi
pamoja na kuingia moja kwa moja katika mashindano ya kugombea Kombe la Kangi.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ambaye pia Mbunge wa Jimbo la Mwibara, Kangi Lugola
akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Busambara, Kata ya Kitengule katika Mkutano wa
hadhara uliofanyika katika Uwanja wa Shule ya Msingi Busambara jimboni humo, Wilaha ya
Bunda, mkoani Mara. Lugola aliwaagiza Polisi wilayani humo kuwakamata wanafunzi watoro
pamoja na wanao warubuni watoto wa kike katika shule mbalimbali wilayani humo.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ambaye pia Mbunge wa Jimbo la Mwibara, Kangi Lugola
(kulia) akimsikiliza mwananchi wa Kijiji cha Busambara, Kata ya Kitengule, Kaitila Jumbula,
alipokua anauliza swali kuhusu maendeleo ya Kata hiyo katika Mkutano wa hadhara uliofanyika
katika Uwanja wa Shule ya Msingi Busambara, jimboni humo, Wilaha ya Bunda, mkoani Mara.
Lugola aliwaagiza Polisi wilyani humo kuwakamata wanafunzi watoro pamoja na wanao
warubuni watoto wa kike katika shule mbalimbali wilayani humo. Picha na Wizara ya Mambo
ya Ndani ya Nchi.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...