NA MWAMVUA MWINYI,MAFIA

MADIWANI wawili kutoka chama cha wananchi (CUF) kata ya Kilindoni na Jibondo ,wilayani Mafia ,Mkoani Pwani, wamejihudhuru nyadhifa zao na kujiunga na Chama Cha Mapinduzi(CCM) ,kutokana na chama tawala kurudisha heshima na kuwa sikivu nchini.

Madiwani hao wamerudi CCM katika ziara ya kamati ya siasa mkoani Pwani ,iliyoweka kambi siku mbili wilayani humo,kutembelea miradi na kukagua utekelezaji wa chama hicho . Aliyekuwa diwani wa Jibondo Hassan Mohammed Hassan ,alisema amefanya maamuzi hayo kutokana na chama walichokuwepo kukosa mwelekeo na kukosa sera zinazojiuza. 

Alisema ,kata ya Jibondo ilikuwa na wafuasi wa CCM ambapo ilipofika 2004 wengi wao walihamia upinzani kutokana na baadhi ya mambo kutokwenda wanavyotaka.“Nampongeza Rais Dk.Magufuli, mkuu wa mkoa wa Pwani, wilaya na CCM Mafia na mkoa kwa juhudi zao katika kuinua uchumi wa nchi na kukuza sekta ya viwanda na uwekezaji” alibainisha Hassan. 


Aliyekuwa diwani wa Jibondo wilayani Mafia Hassan Mohammed Hassan ,akimpa mkono Mwenyekit wa Chama Cha Mapinduzi,Mkoani Pwani Ramadhani Maneno baada ya kujihudhuru nyadhifa yake na kujiunga na Chama Cha Mapinduzi(CCM) (picha na Mwamvua Mwinyi).KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA>>>>

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...