Na Leandra Gabriel, Blogu ya jamii

TIMU ya wanawake kutoka jimbo la Manonga Wilayani Igunga, Mkoani Tabora itaingia rasmi kambini kesho Augusti 13, 2018 kujiandaa na michezo ya kirafiki ili kujiweka sawa na michuano ya ligi daraja la kwanza Tanzania bara inayotarajiwa kuanza kutimua vumbi Septemba 6 mwaka huu.

Akizungumza na Blogu ya jamii msimamizi wa kambi hiyo Bi. Pendo Ndaki ambaye pia ni Mwalimu Mkuu wa shule ya sekondari Ziba ameeleza kuwa Manonga Queens ipo katika hali nzuri sana na wapo tayari kwa mashindano hayo.Ameeleza kuwa timu hiyo inayojiandaa na ligi daraja la kwanza nchini tayari imeanza kujifua vikali kabla michuano hiyo kuanza kwa kuanza kucheza mechi za kirafiki.

Aidha mlezi wa timu hiyo ambaye pia ni Mbunge wa jimbo la Manonga Mh. Seif Khamis Gulamali ameeleza kuwa wamejidhatiti kufuzu kati ya timu mbili zitakazopanda daraja na Ametoa gharama zote za awali kwa ajili ya kambi hiyo ya maandalizi.

Mh.Gulamali amehimiza wadau wengine kujitoa zaidi kwa timu hiyo ili iweze kung'ara kwa kutoa ushirikiano wa hali na mali.Timu 18 zimethibitisha kushiriki Ligi Daraja la Kwanza kwa Wanawake litakaloanza Septemba 6, mwaka huu.

Ligi hiyo itachezwa katika mfumo wa makundi na timu 2 zitapanda daraja wakati zitakazobaki zitasalia kwenye ligi daraja la Kwanza. 

Timu zilizothibitisha ushiriki wao ni:

1.Yanga Princes -Dar es Salaam
2.TSC - Mwanza 
3.Mapinduzi Princess -Tanga 
4.Migoli Queens -Iringa 
5.Ruangwa Queens -Lindi 
6.Viva FC -Mtwara 
7.Singida Warriors -Singida
8.Katoro Queens -Geita 
9.Victoria Queens -Kagera 
10.Tanzanite FC -Arusha 
11.Mapinduzi Queens -Njombe 
12.Allans Queens -Dodoma 
13.Manonga Queens -Tabora
14.Abeehe Bha Kyela FC -Mbeya
15.Kisarawe Queens -Pwani 
16.Testimony -Kilimanjaro 
17.Mbinga Queens -Ruvuma 
18.Kizuka Sekondari -Morogoro 

Timu hizo shiriki ni kwa mujibu wa Afisa habari wa Shirikisho la mpira wa miguu nchini (TFF) Cliford Mario Ndimbo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...