.
Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB Bank, Dk. Charles Kimei, akizungumza na wajasiriamali wa Sido, wakati wa semina yao, iliyofanyika Sido Mkoani, Dar es Salaam mwishoni mwa wiki. Kulia ni Meneja wa Sido Mkoa wa Dar es Salaam, MacDonald Maganga, Ofisa Mtendaja Mkuu wa Kampuni ya Mlako Purified Ice Cubes, Joseph Mlay (kushoto) na Mkurugenzi wa Huduma kwa Wateja wa benki hiyo, Jessica Makhuka.
Baadhi ya wanasemina wajasiriamali, wakimsikiliza Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB Bank, Dk. Charles Kimei, wakati alipowatembelea na kuzungumza nao katika mafunzo yao ya wiki moja, Sido Mkoani Dar es Salaam mwishoni mwa wiki. 
Mwenyekiti wa semina ya wajasiraimali wa Sido, akitoa shukurani kwa Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB Bank, Dk. Charles Kimei. 
Meneja wa Kampuni ya kutengeneza manukato na vipodozi ya efa, Obed Musiba (kulia), akimpatia maelezo Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB Bank, Dk. Charles Kimei (wa pili kulia), kuhusu chupa za vipodozi na manukato zinazotengenezwa na moja ya mashine zao kwenye kiwanda chao. Kushoto ni Meneja wa Sido Mkoa wa Dar es Salaam, MacDonald Maganga.
Mkurugenzi wa Kampuni ya Sido Incubator Programme Star Natural Products, George Buchafwe (kulia), amkimpatia maelezo Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB Bank, Dk. Charles Kimei (katikati), kuhusu vipuri vya mashine za kutengenezea sabuni vinavyotengenezwa na kampuni yake katika Ofisi za Sido Mkoa wa Dar es Salaam, jijini. Kushoto ni Mkurugenzi wa Huduma kwa Wateja wa benki hiyo, Jessica Makhuka. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...