Msanii nyota wa muziki wa kizazi kipya nchini (Bongofleva) na Mkurugenzi wa WCB Nassib Abdull almaarufu Diamond Plutnum akimkabidhi ufunguo wa gari  mshindi wa shindano la 'Nogewa Ushinde' ,Mkazi wa ubungo ndugu Bakari Said,ambaye anajishughulisha na biashara ya kuuza mitumba,kwenye hafla fupi ya mabakabidhiano iliyofanyika leo jijini Dar.


 Shindano hilo ambalo limekuwa likiwavutia vijana wengi kutokana na zawadi mbalimbali ziilizokuwa zikitolewa,limedumu takribani mwezi mmoja sasa kupitia bidhaa za Diamond Karanga,anaeshuhudia kulia ni Afisa Mkaguzi kutoka bodi ya michezo ya kubahatisha Tanzania Bi.Chiku Salehe .

Aidha katika hafla hiyo Mshindi Bakari Saidi alieleza kwa ufupi huku akionekana mwenye furaha tele,kuwa yeye anafanya biashara ya kuuza mitumba Ubungo jijini Dar es salaam,amesema pamoja na kuibuka mshindi bado ataendelea kutumia bidhaa hizo,Bakari akaongeza kuwa gari hilo litamkomboa kiuchumi,kwa sababu ni mara yake ya kwanza kumiliki gari,hivyo atalitumia kwa matumizi yake binafsi na baadae anaweza kuchukua uamuzi mwingine wa kulifanyia biashara ili kujiongezea kipato.
Afisa Mkaguzi kutoka bodi ya michezo ya kubahatisha Tanzania Bi.Chiku Salehe akizungumza machache mbele ya Waandishi wa habari (hawapo pichani) mapema leo kwenye tukio la Muuza Mitumba akikabidhiwa gari yake,baada ya kuibuka mshindi kwenye shindano la 'Nogewa Ushinde' kupitia bidhaa ya Diamond Karanga,Kushoto ni Msanii nyota wa muziki wa kizazi kipya nchini (Bongofleva) na Mkurugenzi wa WCB Nassib Abdull almaarufu Diamond Plutnum na kulia ni Meneja wa WCB Hamis Taletale almaarufu Babutale.

Meneja wa WCB Hamis Taletale almaarufu Babutale akitoa muongozo wa baadhi ya mambo kwa ufupi kabla ya shughuli nzima ya makabidhiano ya Gari kwa mshindi wa bidhaa ya Diamond Karaga kuanza,hafla hiyo imefanyika mapema leo kwenye Ofisi za WCB zilizoko Mbezi Beach jijini Dar  

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...