Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Faustine Ndugulile (wa pili kulia) akipokea Cheti cha Mfumo wa Uhakiki bora wa kiwango cha Kimataifa (ISO 9001:2015) kutoka kwa Muwakilishi wa Taasisi ya BSI (British Standards Institute), Mini Sharma (kushoto) iliyotolewa kwa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF). Wanaoshuhudia ni Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Mfuko huo, Spika wa Bunge Mstaafu, Anna Makinda (wa pili kushoto) pamoja na Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF), Bernard Konga.
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Faustine Ndugulile (katikati) akikabidhi Cheti cha Mfumo wa Uhakiki bora wa kiwango cha Kimataifa (ISO 9001:2015) kwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF), Spika wa Bunge Mstaafu, Anna Makinda kilichotolewa na Taasisi ya BSI (British Standards Institute) kwa Mfuko huo leo Agosti 20, 2018.
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF), Spika wa Bunge Mstaafu, Anna Makinda (katikati) naye alikabidhi cheti hicho kwa Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF), Bernard Konga.
Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF), Bernard Konga akionyesha cheti hicho kwa wageni mbalimbali waliohudhulia hafla hiyo.
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Faustine Ndugulile akizungumza wakati akitoa hotuba yake katika hafla ya kupokea Cheti cha Mfumo wa Uhakiki bora wa kiwango cha Kimataifa (ISO 9001:2015) kilichotolewa na Taasisi ya BSI (British Standards Institute)  Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF), leo Agosti 20, 2018.
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF), Spika wa Bunge Mstaafu, Anna Makinda akifurahi jambo wakati akizungumza katika hafla hiyo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...