Na Woinde Shizza Globu ya jamii ,Arusha

WATALAAM wa manunuzi ya umma nchini wametakiwa kuzingatia  weledi  katika utendaji  wao wa kazi na kuepukana na  vitendo vya ubadhirifu ,rushwa na matumizi mabaya  ya fedha za umma.

Hiyo itasaidia kudhibiti matumizi mabaya ya fedha na  kusaidia   fedha hizo kutumika katika maendeleo mapana zaidi ya Taifa.

Akizungumza kwa niaba ya Rais Dk.John Magufuli wakati akifungua mkutano wa siku tatu wa wataalamu na wabobezi wa manunuzi ya umma(IPPC) kutoka nchini 46 duniani unaofanyika jijini Arusha nchini Tanzania,Waziri wa Fedha na Mipango Dk.Philp Mpango amesema mkutano huo  unalenga kujadiliana namna ya kudhibiti matumizi mabaya ya fedha za umma kupitia taknolojia mpya ya manunuzi .

‘’Ununuzi wa umma ndio sehemu kubwa ambapo fedha za bajeti zinapita, hivyo ukifanyika vibaya maana yake Serikali inapata hasara ndio maana tunasisitiza weredi wa wataalamu wa manunuzi kwa sababu kuna mamunuzi hewa na miradi hewa,"amesema.Aidha amesema asilimia 70 ya fedha za matumizi ya kawaida zinapitia ununuzi wa umma na asilimia 100 ya bajeti  ya fedha zote za maendeleo zinapitia manunuzi ya umma ,hivyo bajeti zote katika maeneo hayo mawili zikitumika vibaya lazima serikali iumie.
Waziri wa Fedha na Mipango Dkt.Philip Mpango akisalimiana na mwenyekiti wa bodi ya manunuzi Dkt. Hellen Bandiho wakati wa ufunguzi wa mkutano wa wabobezi na wanunuzi wa umma jana ,uliofanyika katika ukumbi wa simba uliopo ndani ya jengo la mikutano la AICC .
Dkt Mpango akifungua mkutano wa siku tatu unaohusu bodi ya manunuzi, jana jijini Arusha 
Washiriki wa mkutano huo wakifuatilia yaliyokuwa yakijiri ndani ya mkutao huo 
waziri Dkt Mpangao akiwa katika picha ya pamoja na wakuu wa taasisi zilizopo chini ya taasisi ya wizara ya fedha na mipango(picha zote na Woinde Shizza,Glob ya jamii Arusha.HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...