Na Said Mwishehe, Globu ya jamii 

WAZIRI wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa Joyce Ndalichako ametoa maagizo kwa Baraza la Elimu ya Ufundi(Nacte)kutosita kuchukua hatua ikiwamo ya kuvifuta vyuo ambavyo vitabainika kutoa elimu kwa ubabaishaji.

Pia amelishauri Baraza hilo kuhakikisha linasimamia na kutoa muongozo kuhusu program mbalimbali za utoaji elimu ya ufundi ambayo ametaka iwe inaendana na soko la ajira nchini ili kuhakikisha Watanzania wanapata fursa ya kuajiriwa kwa ajili ya kufanya kazi katika miradi mikubwa inayoendelea nchini.

Profesa Ndalichako ameyasema hayo leo jijini Dar es Salaam wakati anazindua rasmi Baraza la Uongozi la Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi nchini ambalo Mwenyekiti wake ni Profesa John Kandoro.

Kuhusu vyuo ambavyo vinashindwa kutoa elimu bora, Profesa Ndalichako amesema baraza hilo lisisite kuchukua hatua ikiwamo ya kuvifutia usajili vyuo ambavyo vitabainika kushindwa kukidhi vigezo vilivyowekwa.

Amefafanua haiwezekani vijana wawe wanalipa fedha kwenye vyuo ambavyo elimu wanayotoa ni ya ubabaishaji na kwamba hilo halikubaliki na lazima hatua zichukuliwe.

“Kuna vyuo ambavyo vipo kwa ajili ya kuunga mkono jitihada za Serikali za kutoa elimu bora lakini pia kuna vyuo ambavyo vimeanzishwa kwa ajili ya biashara na hivyo ndivyo vyenye matatizo.“Kama kuna mtu aliamua kuwekeza kwenye kunzisha chuo kwa ajili ya kufanyabiashara basi atambue ni bora atafute kazi nyingine ya kufanya na sio hiyo tena,”amesema Profesa Ndalichako.
 Waziri wa Elimu,Sayansi na Teknolojia Profesa Joyce Ndalichako akizungunza leo jijini Dar es Salaam wakati anazindua rasmi Baraza la Uongozi la Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi
 Baadhi ya washiriki kwenye uzinduzi wa Baraza la Uongozi la Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi wakimsikiliza mgeni rasmi Waziri wa Elimu,Sayansi na Teknolojia Profesa Joyce Ndalichako(hayupo pichani).
 Mkurugenzi wa Nacte akizungumza leo jijini Dar es Salaam wakati wa uzinduzi wa Baraza la Uongozi la Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi.
Mwenyekiti wa Baraza la Uongozi wa Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi Profesa John Kandoro akizungumza leo jijini Dar es Salaam wakati wa uzinduzi wa Baraza hilo.KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA>>>>>

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...