WAZIRI wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto Ummy Mwalimu amesema wizara yake itaendelea kukarabati na kupanua vyuo vya mafunzo ya afya kada ya kati nchini ili kuweza kuongeza udahili kwa wanafunzi wanaofaulu kwenye masomo ya sekondari wenye vigezo vya kuingia kwenye vyuo hivyo. 

Aliyasemma hayo leo wakati halfa ya uzinduzi na makabidhiano ya Majengo ya chuo cha Uuguzi Tanga yaliyojengwa kupitia ufadhili wa mfuko wa Dunia wa Kupambana na Ukimwi Kifua Kikuu na Malaria (Global Fund) alisema kwani ukarabati huo utasaidia kuongeza idadi kubwa ya wanafunzi watakaokuwa wakipata fursa ya kusoma kwenye vyuo hivyo. 

Alisema kutokana na ukarabati huo kwenye chuo cha Uuguzi mkoani Tanga idadi ya wanafunzi wanaodahiliwa kwenye chuo hicho imeongezeka kutoka wanafunzi kutoka 190 hadi 260 ambao wameweza kupata fursa mafunzo kwenye chuo hicho ambao watasaidia kwenye kada hiyo muhimu kwa ustawi wa maendeleo. 

“Kutokana na ukarabati wa majengo haya nimeambiwa na Mkuu wa Chuo kwamba udahili wa wanafunzi kutoka 190 hadi 260 wameweza kutoa fursa kwa vijana wao kuweza kupata nafasi ya kupata mafunzo ya afya kada ya kati huwa naambiwa kwamba na dkt Guwele ambaye ni mkuu wa idara ya mafunzo na afya kada ya kati anasema wanafunzi wengi wanafaulu lakini hawapati mahali pa kuwapeleka sababu kubwa zikiwa ni miundombinu na uchakavu wa majengo na inaumiza vijana wamefaulu vizuri sana lakini hakuna nafasi“Alisema. 

“Lakini tunawashukuru Global Fund kwa ujenzi wa majengo hayo yameweza kusaidia kuongeza udahili hivyo niagize msije mkaacha wanafunzi kwa kusema hakuna nafasi..Wanafunzi waliofaulu kwenye masomo ya sekondari wenye vigezo vya kuingia kwenye vyuo vya mafunzo wachukuliwe wote wasiachwe majumbani “Alisema. 
 WAZIRI wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee wa Watoto Ummy Mwalimu katika akitata utepe kuashiria uzinduzi na makabidhiano ya majengo ya chuo cha Uuguzi Tanga yaliyojengwa kupitia ufadhili wa Mfuko wa Dunia wa Kupambana na Ukimwi Kifua Kikuu na Malaria (Global Fund) kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Tanga Martine Shigella na Mkuu wa Chuo hicho Leah Makala
 WAZIRI wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee wa Watoto Ummy Mwalimu akizungumza wakati wa uzinduzi na makabidhiano ya majengo ya chuo cha Uuguzi Tanga yaliyojengwa kupitia ufadhili wa Mfuko wa Dunia wa Kupambana na Ukimwi Kifua Kikuu na Malaria (Global Fund) 
 Katikati ni Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Ummy Mwalimu akiangalia namna wanafunzi wanavyojifunza kwa vitendo kumfanyia mazoezi mtoto ambaye amezaliwa akiwa hapumui vizuri 
Sehemu ya wananchi waliojitokeza kwenye uzinduzi huo



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...