Na Agness Francis, Globu ya jamii

UONGOZI wa Kikosi cha Azam chini ya  Kocha Mkuu wake Hans Van der Pluijm umesema kwa mazoezi waliyofanya sasa vijana  wapo tayari kupambana dhidi ya Biashara United.

Mchezo huo unatarajiwa kufanyika  leo saa 10 jioni katika dimba la Karume mkoani Mara.

Hivyo Azam mchezo huo wa leo ni wa nne  kwao katika Ligi Kuu Tanzania Bara na wanashika nafasi ya pili wakiwa na alama saba.

Wakati timu ya  Biashara ni  mzunguko wa tano na wanashika nafasi ya 12 ikiwa na alama nne.

Ambapo JKT Tanzania  wakiwa vinara wa ligi hiyo ambayo imeshacheza michezo 4 mpaka sasa na wakiwa na alama 8.

Katika mchezo uliopita Azam FC ilionesha kulazimisha sare  ya kufungana 1-1 dhidi  Mwadui FC katika uwanja wa Kambarage huko mkoani Shinyanga.

Wakizungumzia mchezo wa leo dhidi ya Biashara ,Uongozi wa Kikosi cha Azam umesema wachezaji wao wako vizuri na  hakuna majeruhi.

Wameongeza wachezaji wao kila mmoja akiwa na morali ya kuondoka na alama tatu  ugenini.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...