Na Agness Francis, Globu ya jamii
UONGOZI wa Kikosi cha Azam chini ya Kocha Mkuu wake Hans Van der Pluijm umesema kwa mazoezi waliyofanya sasa vijana wapo tayari kupambana dhidi ya Biashara United.
Mchezo huo unatarajiwa kufanyika leo saa 10 jioni katika dimba la Karume mkoani Mara.
Hivyo Azam mchezo huo wa leo ni wa nne kwao katika Ligi Kuu Tanzania Bara na wanashika nafasi ya pili wakiwa na alama saba.
Wakati timu ya Biashara ni mzunguko wa tano na wanashika nafasi ya 12 ikiwa na alama nne.
Ambapo JKT Tanzania wakiwa vinara wa ligi hiyo ambayo imeshacheza michezo 4 mpaka sasa na wakiwa na alama 8.
Katika mchezo uliopita Azam FC ilionesha kulazimisha sare ya kufungana 1-1 dhidi Mwadui FC katika uwanja wa Kambarage huko mkoani Shinyanga.
Wakizungumzia mchezo wa leo dhidi ya Biashara ,Uongozi wa Kikosi cha Azam umesema wachezaji wao wako vizuri na hakuna majeruhi.
Wameongeza wachezaji wao kila mmoja akiwa na morali ya kuondoka na alama tatu ugenini.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...