Cassius O. Mdami ni miaka miwili sasa tangu umetuacha familia yako; mke wako Rose Mdami; na watoto wako Martina, Grace, Gideon, Gonsalver na Gibson. 
Kila uchao hatuachi kuisikia sauti yako na kukumbuka ucheshi wako kila mara ulipokuwa nasi. Kifo kimetutenganisha nawe. 
 Mungu anajua maumivu yote na machungu tuliyopitia familia yako na tunayoendelea kuyapitia kwa kutokuwepo kwako. Machozi yanatudondoka na hakuna wa kuyafuta; ila tumaini tunalo ya kwamba iko siku moja tutaonana nawe katika makao ya Baba Mbinguni.
Mungu endelea kutufariji kama maneno yako yasemavyo katika kitabu cha Kumbukumbu la Torati 31:8 “ Naye Bwana ndiye atakayekutangulia, atakuwa pamoja nawe, hatakupungukia wala kukuacha; usiogope wala usifadhaike ”
 Pumzika kwa Amani Baba G4

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...