Mkuu wa Mkoa Arusha, Mrisho Gambo (kushoto) akizungumza
na wakazi wa Kimondolosi, wilaya ya Arusha mjini, wakati wa
ziara ya Waziri wa Nishati, Dkt, Medard Kalemani (katikati) ya
kukagua utekelezaji wa mradi wa kusambaza umeme vijijini
(REAIII) wilayani humo.
Waziri wa Nishati, Dkt. Medard Kalemani, akizungumza na
wakazi Kijiji cha Kimondolosi Kata Olasiti Wilaya ya Arusha mjini.
Wakazi wa Kata ya Olasiti, wakimsikiliza Waziri wa Nishati, Dkt.
Medard Kalemani aliyekuwa akizungumza kuhusu kuwapatia
huduma ya umeme.
Waziri wa Nishati, Dkt.Medard Kalemani (wa Tatu kushoto)
akikagua nguzo za umeme katika Kata ya Terati, zitakazotumika
kuwapatia Umeme wananchi wa eneo hilo mkoani Arusha. Wa
Pili kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo.
Na Zuena Msuya, Arusha.
Waziri wa Nishati, Dkt. Medard Kalemani ametoa mwezi mmoja
kwa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) kuhakikisha kuwa
vijiji vyote vilivyopo katika Jiji la wa Arusha vinaunganishwa na
huduma ya umeme. Dkt. Kalemani alitoa agizo hilo jijini Arusha baada ya kukagua
utekelezaji wa mradi wa kusambaza umeme vijijini (REA III)
katika Vijiji vilivyopo jijini humo na kujionea hali ya ukosefu wa
nishati ya umeme.
Dkt. Kalemani alisema kuwa, Wananchi hawafurahii
kucheleweshewa kupata huduma ya umeme hali ya kuwa
wengine walikwishalipia huduma hiyo.
" Haipendezi na haifurahishi machoni mtu kajitahidi kujibana na
kujenga nyumba yake nzuri na ya kisasa, lakini anakosa umeme
wakati uwezo wa kumuunganishia upon a vifaa vipo, sasa kwa
nini asiunganishwe.?," alihoji Dkt. Kalemani.
Kutokana na hali hiyo, aliwataka TANESCO kuunda vikosi kazi
mbalimbali vitakavyosaidia kazi ya kusambaza umeme kwa
wananchi kwa haraka.
Aidha, alimwagiza mkandarasi anayesambaza umeme jijini humo,
kampuni ya Nipo Group, kuhakikisha kuwa anawafungia umeme
wananchi wa Kimondorosi katika Kata ya Olasiti mkoani Arusha
na kuhakikisha kuwa kila siku anatoa ripoti ya utekelezaji wa
mradi kwa mtendaji wa mtaa huo hadi atakapomaliza kuweka
umeme kwa wananchi .
Alisema kuwa, mkandarasi huyo anapaswa kufanya kazi hiyo ili
kuwaondolea kero ya ukosefu wa umeme wananchi hao ambao
wamekaa kwa muda mrefu bila kupata huduma hiyo.
Naye Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo alimshukuru
Waziri wa Nishati kwa kutoa agizo hilo litakalopelekea wananchi
hao kupata umeme kwani wananchi hao walishamlalamikia
kuhusu kukosa huduma hiyo.
Vilevile, mmoja wa wananchi katika Kata hiyo, Clementina Mushi
alimuomba Waziri wa Nishati kuhakikisha kuwa umeme huo
unafika kwa wananchi wote bila kurukwa.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...