Na Ripota Wetu,Michuzi Blog

MBUNGE wa Mtama Nape Nnauye(CCM) amenusurika kifo baada ya gari aliyokuwa akisafiria kupata ajali.

 Nape amepata ajali hiyo leo asubuhi katika Kijiji cha Kibutuka akiwa njiani kuelekea Liwale kwa ajili ya kushiriki kikao cha Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi(CCM)Mkoa.

Taarifa ambazo Michuzi Blog imezipata asubuhi zinaeleza kuwa ndani ya gari hiyo Nape alikuwa ameambatana na watu wengine wanne ambao wote ni wazima na hamna aliyedhurika. 
Mbunge wa Jimbo la Mtama mkoani Lindi amepata ajali akiwa safarini kuelekea wilayani Liwale kushiriki kikao cha kamati kuu ya siasa ya mkoa wa Lindi ikiwa ni pamoja na kuungana  na ziara ya Katibu mkuu wa CCM Taifa Bashiru Ally anayoifanya wilayani Liwale. Katika ajali hiyo hakuna kifo
Baadhi ya wakazi wa Kijiji cha Kibutuka wakilitazama Gari lenye namba za usajiri T 349 DEL likiwa limepinduka  

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...