NA MWAMVUA MWINYI, KIBITI .

NAIBU Waziri wa Nishati ,Subira Mgalu amethibitisha kuwa serikali inaendelea kujenga gati la Nyamisati, Kibiti, mkoani Pwani na haina mpango wa kulihamisha ambapo linatarajiwa kugharimu sh. bilioni 14 hadi kukamilika kwake. 

Amewatoa shaka hiyo wananchi ambao walikuwa wakidai ujio wa ujenzi wa mradi mkubwa wa uzalishaji umeme katika maporomoko ya mto Rufiji, Hydro Power (Stigilers Gorge )unaweza kusababisha athari za ujenzi wa gati hilo kwenda kisiwa cha Mafia. 

Subira aliyasema hayo, wakati akizungumza na wananchi wa Nyamisati,  mara baada ya kutembelea ujenzi wa gati hilo .Alisema  mradi wa ujenzi wa gati hilo umefanyiwa utafiti wa kina na kubaini  hautakuwa na athari zozote za kimazingira .

Subira alieleza, baadhi ya watu wanadai kuwa eneo hilo la gati kina cha maji kitapungua suala ambalo sio la kweli ."Wataalamu wa mradi wa Hydro Power na gati walikaa kubadilishana uzoefu, na ripoti yao inaonyesha hakutakuwa  na athari za kimazingira "
  Naibu waziri wa nishati, Subira Mgalu akizungumza na wananchi wa Nyamisati wilayani Kibiti.

Naibu waziri wa nishati, Subira Mgalu (wa pili kutoka kulia)  akimuelekeza jambo meneja wa ujenzi wa mradi wa gati la Nyamisati kutoka mamlaka ya usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA), Mhandisi Erick Madinda (kushoto) kabla ya waziri huyo kuzungumza na wananchi wa Nyamisati wilayani Kibiti.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA>>>>>

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...