Na Ripota Wetu,Globu ya jamii
OFISA Mtendaji Mkuu wa DAWASA Mhandisi Cyprian Luhemeja ametembelea mradi wa maji wa Chalinze ili kujionea maendeleo ya mradi na kupanga utaratibu wa kuongeza kasi ya ujenzi.
Ametembelea mradi huo ikiwa ni siku yake ya nne tangu kutangazwa rasmi Septemba 8 mwaka, amefanya maamuzi ya kuongeza nguvu katika usimamizi na kutaka mkandarasi wa Kampuni ya OIA ya India kutekeleza kazi usiku na mchana ili kuleta matokeo yanayotarajiwa.
Akizungumzia mradi huo Mhandisi Luhemeja amesema mradi utazinduliwa Desemba mwaka 2018.
Leo pia anaendelea na ziara katika miradi ya usambazaji maji.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...