Na Asha Ngoma
Taasisi ya Tanzanite Founder Foundation na mvumbuzi wa madini ya Tanzanite Mzee Jumanne Mhero Ngoma wameadhimisha  miaka 51 tangu madini hayo yagunduliwe mwaka 1967 katika hotel ya Serena Hotel jijini Dar es salaam leo Septemba 23, 2018.
Hata hivyo sherehe hizo hazikuwa na shamrashamra zilizoandaliwa na badala yake ukafanyika mkutano na wanahabari  baada ya kuahirisha sherehe hizo kutokana na maombolezo ya kitaifa ya kuzama kwa kivuko cha MV Nyerere huko Ukara, Mkoani Mwanza.
Tanzanite Founder Foundation ni Taasisi isiyo ya kiserikali lilioanzishwa na kusajiliwa mwaka 2013 ikiwa na lengo kuu la kuwajengea uwezo vijana na watu wote waishio migodini na maeneo jirani ili kuboresha na kuongeza ufanisi katika shughuli zao za kila siku kutokana na madini haya. Tanzanite Founder Foundation na wadau leo
imeona iadhimishe miaka 51 tangu madini haya ya kipekee duniani kuvumbuliwa nchini Tanzania. 
Madini haya husheherekewa ulimwenguni na mashirika, taasisi na wafanya biashara Mbalimbali wa madini lakini hayajawahi kusherehekewa wala kuadhimishwa nchini Tanzania. Kwa mara ya kwanza Taasisi ya Tanzanite Founder Foundation imeona iadhimishe siku hii kwa kutoa taarifa kwa vyombo vya habari kuhusu madini haya ikiwa ni pamoja na kutoa historia fupi ili kutoa tathmini ya tulipotoka na tulipo kwa sasa ikiwa ni pamoja na kudhihirishia ulimwengu kuwa Tanzanite ni fahari yetu na urithi wetu watanzania. 
Madini ya Tanzanite yalivumbuliwa mwaka wa 1967 na Mzee Jumanne Mhero Ngoma ambaye ni Mtanzania, a iyaokota madini haya katika eneo la Mirerani Wilaya ya Simanjiro Mkoa wa Arusha wakati huo na kuyapeleka kwa ofisi ya Madini Moshi Mkoa wa Kilimanjaro ambayo nayo hawakuyatambua ni madini gani.
Bango la miaka 51 tangu madini hayo yagunduliwe mwaka 1967 huko Mirerani kwenya mkutano na wanahabari katika hotel ya Serena Hotel jijini Dar es salaam leo.
Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Tanzanite Founder Foundation Bi. Asha Ngoma akiwa na mvumbuzi wa madini ya Tanzanite Mzee Jumanne Mhero Ngoma (wa pili kushoto) na watendaji wa taasisi hiyo  katika mkutano na wanahabari katika kuadhimisha   miaka 51 tangu madini hayo yagunduliwe mwaka 1967 huko Mirerani. Mkutano huo umefanyika leo katika hotel ya Serena jijini Dar es salaam.
Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Tanzanite Founder Foundation Bi. Asha Ngoma akipongezana  na mvumbuzi wa madini ya Tanzanite Mzee Jumanne Mhero Ngoma
Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Tanzanite Founder Foundation Bi. Asha Ngoma akiwa na mvumbuzi wa madini ya Tanzanite Mzee Jumanne Mhero Ngoma. Kusoma habari kamili BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...