Viongozi wa Kimila kutoka Jamii ya Kimasai Tanzania wamlilia Waziri
Mwakyembe kuhusu eneo la kufanyia Mikutano ya Kimila.
 Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Dkt.Harrison
Mwakyembe (watatu kutoka kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na
viongozi wa Kimila kutoka jamii ya Kimasai nchini akiwa ameshikana
mkono na Mwenyekiti wa Umoja wa Machifu wa Kimasai Tanzania Chifu.
Isack Meijo Ole Kisongo (wapili kulia) mara baada ya viongozi hao
kuwasilisha malalamiko yao leo Jijini Dodoma kuhusu mgogoro wa eneo
la kufanyia mikutano ya kimila lililoko Mjini Arusha kupunguzwa pamoja
na jengo lao walilojengwa kusimamishwa ujenzi kwa zaidi ya miaka kumi
hivyo kusababisha changamoto ya utekelezaji wa shughuli zao za
kimila,wa kwanza kushoto ni Mwenyekiti wa Ukoo wa Laizer Tanzania
Bw.Oltetiai Sozi,anayemfuata (wapili kushoto) ni Mwenyekiti wa Ukoo wa
Mollel Tanzania Bw.Saitabau Mollel, kutoka kushoto wa kwanza ni
Mwenyekiti wa Kamati ya Dira kwa Jamii ya Kimasai Tanzania Zablon Ole
Muterian.
 Mwenyekiti wa Kamati ya Dira kwa Jamii ya Kimasai Tanzania Bw.
Zablon Ole Muterian (kulia) akimwonyesha Mheshimiwa Waziri wa Habari
Utamaduni Sanaa na Michezo Dkt.Harrison Mwakyembe ( baadhi ya nakala
za barua,taarifa na picha zinazohusu mgogoro wa eneo lao la kufanyia
mikutano ya kimila kwa jamii ya Kimasai nchini lililopo Arusha Mjini
namna lilivyopunguzwa na zuio la kujenga ukumbi wao wa mikutano
ulivyofanyika na kusababisha kero kwao wakati wa kufanya mikutano yao
ya kimila kitaifa kwa kila mwezi katika kikao kilichoendeshwa na
Mheshimiwa Waziri,wakiwemo viongozi wa Idara ya Utamaduni pamoja na
wazee hao wa kimila kilichofanyika leo jijini Dodoma.
Viongozi wa Kimila kutoka Jamii ya Kimasai Tanzania wakimsikiliza
kwa makini Mheshimiwa Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo
Dkt.Harrison Mwakyembe (hayupo pichani) alipokuwa akiwaeleza hatua
atakazo chukua katika kufanikisha anatatua mgogoro wao kuhusu eneo lao
la kufanyia shughuli za kimila lililopo Mjini Arusha, leo Jijini Dodoma
mara baada ya wazee hao kumweleza changamoto wanazozipata katika
kuendesha shughuli za za kimila tangu ya eneo hilo lilipopunguzwa.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...