Na Veronica Kazimoto-Tanga
Wafanyabiashara mkoani Tanga wameelimishwa kuhusu Msamaha wa Riba na Adhabu ya Malimbikizo ya Madeni ya Kodi, Mabadiliko ya Sheria za Kodi ya Mwaka 2018 na Mfumo wa Maadili wa Watumishi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kwa lengo la kuwawezesha wafanyabiashara hao kujua kwa undani masuala yanayohusu kodi pamoja na kuwahi kuomba msamaha wa riba na adhabu ambapo mwisho wa kutuma maombi ni tarehe 30 Novemba, 2018.

Akifungua semina ya wafanyabiashara hao mkoani hapa iliyoandaliwa na TRA, Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa Monica Kinara amesema kuwa, elimu hiyo imekuja wakati muafaka na siyo tu itawasaidia kujua masuala ya kodi bali wale wenye malimbikizo ya madeni ya kodi watanufaika na msamaha huo na hatimaye wataweza kulipa kodi kwa wakati.

"Ninawashukuru sana TRA kwa kuleta elimu hii hapa mkoani kwetu na ni matumaini yangu kuwa, wafanyabiashara mtatumia fursa hii vizuri ili iwasaidie kuelewa masuala mbalimbali yanayohusu kodi na hasa msamaha wa riba na adhabu ya kodi ili muweze kuomba msamaha huo ndani ya muda uliopangwa," alisema Kinara.

Naye, Meneja wa Elimu kwa Mlipakodi kutoka TRA Makao Makuu Diana Masalla amewaeleza wafanyabiashara hao kwamba, ni jukumu la kila mwenye malimbikizo ya madeni ya kodi kuwahi kuomba msamaha wa riba na adhabu akiwa ameambatisha dodoso maalum la msamaha huo pamoja na ritani ya taarifa za Mlipakodi.
 Meneja wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Mkoa wa Tanga Masawa Masatu akizungumza wakati wa semina ya wafanyabiashara  iliyofanyika  jijini Tanga kwa lengo la kutoa elimu ya Msamaha wa Riba na Adhabu ya Malimbikizo ya Madeni ya Kodi, Mabadiliko ya Sheria za Kodi ya Mwaka 2018 pamoja na Maadili ambapo takribani wafanyabiashara 150 wamehudhuria semina hiyo.
 Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Tanga Monica Kinara akizungumza wakati wa semina ya wafanyabiashara iliyofanyika  jijini Tanga kwa lengo la kutoa elimu ya Msamaha wa Riba na Adhabu ya Malimbikizo ya Madeni ya Kodi, Mabadiliko ya Sheria za Kodi ya Mwaka 2018 pamoja na Maadili ambapo takribani wafanyabiashara 150 wamehudhuria semina hiyo.
 Meneja wa Elimu kwa Mlipakodi Diana Masalla kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Makao Makuu akiwasilisha mada kuhusu Mabadiliko ya Sheria za Kodi wakati wa semina ya wafanyabiashara iliyofanyika  jijini Tanga kwa lengo la kutoa elimu ya Msamaha wa Riba na Adhabu ya Malimbikizo ya Madeni ya Kodi, Mabadiliko ya Sheria za Kodi ya Mwaka 2018 pamoja na Maadili ambapo takribani wafanyabiashara 150 wamehudhuria semina hiyo.
 Afisa Maadili Mwandamizi Adelaida Rweikiza kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Makao Makuu akiwasilisha mada kuhusu Mfumo wa Maadili wa Watumishi wa TRA wakati wa semina ya wafanyabiashara iliyofanyika  jijini Tanga kwa lengo la kutoa elimu ya Msamaha wa Riba na Adhabu ya Malimbikizo ya Madeni ya Kodi, Mabadiliko ya Sheria za Kodi ya Mwaka 2018 pamoja na Maadili ambapo takribani wafanyabiashara 150 wamehudhuria semina hiyo.

Baadhi ya wafanyabiashara waliohudhuria semina iliyoandaliwa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) jijini Tanga kwa lengo la kutoa elimu ya Msamaha wa Riba na Adhabu ya Malimbikizo ya Madeni ya Kodi, Mabadiliko ya Sheria za Kodi ya Mwaka 2018 pamoja na Maadili ambapo takribani wafanyabiashara 150 wamehudhuria semina hiyo.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...