Profesa Marjorie Mbilinyi akizungumzia simulizi ya hadithi yake  Jijini Dar es Salam katika viwanja vya ofisi ya TGNP mtandao  jinsi alivyofanikiwa  kupambana kupiga vita mfumo dume usimtawale katika kutimiza ndoto zake.
 rofesa Ruth Meena kushoto akimsikiliza kwa makini profesa Marjorie Mbilinyi  Jijini Dar es salaam wakati wa kusimulia hadithi ya harakati za mapambano ya kujikwamua kuondokana mfumo dume.
Profesa Ruth Meena akiwa  anawasimulia hadithi  Wanafunzi wa vyuo vikuu  Mbali mbali na wageni waalikwa  Jijini Dar es Salaam namna alivyokuwa mwanaharakati wa kukataa kudidimizwa  katika kujikwamua Kama mwanamke katika kujiendeleza  kimasomo  huku akiwa na majukumu ya kuangalia familia,pamoja na kufanya kazi.

Na Agness Francis,blogu ya jamii.
KATIKA harakati za ukombozi wa mwanawake,wanawake wametakiwa kuwa kipaumbele katika kuondokana na mfumo dume uliotawala katika jami yetu.

Ambapo wanatakiwa kuwa mstari wa mbele kuukataa  na kupiga vita ukatili wa kijinsia,utabaka pamoja na ubeberu uliokithiri hasa kwa zile familia ambazo bado zinadhana  potofu ya kumdidimiza mwanamke katika kupata Elimu na uongozi.

Amesema hayo  Jijini Dar es Salaam katika viwanja vya TGNP mtandao  Profesa  Marjorie Mbilinyi  wakati wa kilinge cha simulizi za hadithi za maisha yake alivyopambana mpaka hapo alipofikia pamoja na misuko suko yote aliyopitia akipindi akiwa binti mdogo lakini alihakikisha anaepukana na janga la kukandamizwa Kama mwanamke.

Profesa mbili ambaye ni mwanaharakati wa mabadiliko ya  ukombozi wa mwanamke kimapinduzi  wakati wa simulizi amesema kuwa hakuna utofauti sana wa ubaguzi huo hapa nchini kwetu na ulaya.

"Isipokuwa  wanawake wa nchi za nje wamepiga hatua katika kujikomboa kuondokana na utabaka,ubepari,hivyo na sisi tujifunze kutoka kwao" amesema Profesa Mbilinyi.

Aidha mwanaharakati profesa Ruth Meena wakati wa simulizi wa hadithi yake amesisitiza kuwa  wanawake wapige vikali vita ya  mfumo huo wa unyonywaji na amewataka kusimama imara  kupigania maendeleo na kutimiza ndoto zao.

Hata hivyo mwanafunzi wa chuo kikuu cha Mlimani  Sliyvia Sostenes baada ya  simulizi hiyo amesema kuwa watakuwa mabalozi wazuri katika kuwaelemisha wengine ambao wapo katika janga hilo ili kuleta ukombozi wa mwanamke kimapinduzi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...