Waziri wan chi Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na serikali za mitaa (TAMISEMI )Selemani Jafo akizungumza na baadhi ya madereva na makondakta wanaofanya kazi zao katika stendi ya mabasi ya Wilayani Bagamoyo wakati wa alipofanya ziara yake ya kikazi ya kushitukiza kwa lengo la kusikiliza changamoto ya miundombinu ya vyoo inayowakabili na kuwalazimu kujisaidia katika mifuko ya plastiki pamoja na vichakani .
NA VICTOR MASANGU, BAGAMOYO
WAZIRI wan chi ofisi ya Rais Tawala za mikoa na serikali za mitaa (TAMISEMI) Selemani Jafo amefanya ziara ya kushitukiza katika stendi ya mabasi ya Wilayani Bagamoyo na kubaini kufungwa kwa choo kwa zaidi ya siku tatu bila ya kutumika kutokana na shimo lake kujaa maji na kupelekea baadhi ya madereva,makondakta pamoja na abiria kupata usumbufu mkubwa na kuamua kujisaidia katika mifuko ya plastiki aja kubwa na ndogo na kwenda kuitupa kandokando ya barabara na wengine kujisaidia vichakani.
Jafo aliweza kubaini kuwepo kwa changamoto hiyo ambapo amesema kwamba katika eneo la stedi hiyo ya mabasi kuna mapugufu mengi katika suala zima la miundombinu ya vyoo,pamoja na kuwepo kwa miundombinu mibovu ya barabara kutokana na kuwa na mashimo hivyo kuwapa wakati mgumu madereva katika utekelezaji wa majukumu yao.
Pia waziri Jafo ametoa muda wa siku mbili kwa maafisa wa mazingira pamoja na afya wa Wilayani Bagamoyo kumwandikia barua ya maelezo kuhusiana na saakata la kukithiri kwa uchafu huo sambamba na kumwagiza Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo kuunda tume kwa ajili ya kuweza kuchunguza kwa kina kuhusiana na baaadhi ya watu ambao wanafanya hujuma na kusababisha upotevu wa fedha za ushuru wa mabasi katika stendi hiyo.
“Kwa kweli hii hali mimi siwezi kuivumilia kabisa hata kidogo maana nimepata taarifa kwamba stedi hii inachangamoto mbali mbali lakini kubwa zaidi ni kufungwa kwa choo kwa zaidi ya siku tatu kutokana na kuwa ni kibovu, kwa hiyo sasa watu wanaangaika kweli kweli mpaka wanaamua sasa kwenda kujisaidia vichakani na kama haitoshi wengine wanatumia mifuko ya plastiki alafu wanakwenda kitupa hii sio sahihi hata kidogo,”alisema Jafo.
Kadhalika Jafo aliongeza kuwa kutokana na kukithiri kwa uchafu katika stendi hiyo ya mabasi kunaweza kusaababsiha mlipuko wa magonjwa mbali mbali hivyo kunahitajika juhudi za makusudi kutoka kwa wataalamu wa afya pamoja na mazingira zinafanyike haraka san ili kuweza kukabiliana na hali hiyo ambayo imekuwa ni kero kwa wananchi.
Nao baadhi ya madereva hawakusita kutoa kilio chao kwa Waziri Japo ambapo wamedai kuwa wamekuwa wakipata usumbufu mkubwa pindi wanapohitaji huduma ya kujisaidia na kwamba kwa sasa wapo katika mazingira hatarishi ya kupata magonjwa ya mlipuko kutokana na kukithiri kwa watu kujisaidia ovyo katika maeneo ambayo sio rasmi.
Aidha katika hatua nyingine Waziri Jafo katika ziara yake hiyo ya kikazi aliweza kutembelea hospitali ya Wilaya ya Bagamoyo n akuonyesha masikitiko yake makubwa kutokana na uzembe unaofanywa na baadhi ya watendaji, na kutoa muda wa siku 30 kwa mkurugenzi wa halmashauri hiyo kuhakikisha anatekeleza agizo lake alilolitoa la hospitali zote nchini kufunga mfumo wa kielekitroniki wa ukusanyaji wa mapato unaofahamika kwa jina la Got Homis.
STENDI ya mabasi ya Wilayani Bagamoyo Mkoani Pwani imekuwa ikilalamikiwa kwa kipindi kirefu kutokana na kuwepo kwa changamoto mbali mbali zinazoikabili ikiwemo kuwepo kwa miundombinu mibovu ya vyoo,ambayo inachangia kwa kiasi kikubwa kusababisha usumbufu mkubwa kwa watumiaji hususan madereva,makondakta pamoja na abiria na kupelekea kuamua kujisaidia katika maeneo ambayo sio rasmi.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...