Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi alisema wakati umefika kwa Serikali Kuu kwa kushirikiana na Taasisi na Mashirika megine ya Kitaifa na Kimataifa kujenga Kituo cha Taifa kitakacholenga kuwahudumia Watu wenye ulemavu katika kuwajengea nguvu na maarifa ya kuendelea kujitegemea Kimaisha.
Alisema Ulimwengu wa sasa umebadilika kwa kubeba harakati nyingi zinazoibua matukio mbalimbali yanayosababisa Jamii kukumbwa na ajali tofauti katokana na kasi ya maisha na hatimae kuzalisha Walemavu wanaohitaji huduma za matunzo na maarifa mengine ya Kimaisha.
Balozi Seif Ali Iddi alisema hayo wakati wa hafla maalum ya kuzindua rasmi Kituo cha Jumuiya ya Watu wenye Ulemavu cha Jimbo la Shaurimoyo kiliopo pembezoni mwa Skuli ya Sekondari ya Ufundi Mikunguni Mjini Zanzibar.
Alisema tabia ya kuwatenga Watu wenye Ulemavu haipendezi na nidhambi jambo ambalo halikubaliki katika Jamii yoyote ile. Hivyo aliwahimiza wahusika hao wasikubali kukata tamaa katika kupigania haki zao.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar aliushukuru Uongozi wa Kampuni ya Peny Royal na Kumpongeza Mwakilishi wa Jimbo la Shaurimoyo kwa jitihada zao zilizopelekea kujengwa kw kituo hicho muhimu kwa Watu wenye mahitaji Maalum.
Balozi Seif alifarajika kuona kwamba Ujenzi wa Kituo hicho umelenga kuwajengea Uwezo na maarifa Watu wenye Ulemavu wa Jimbo la Shaurimoyo ili wawe Wajasiri Amali watakaokuwa na nguvu za kujiendesha wenyewe Kimaisha.
Makamu
wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akikizindua Rasmi
Kituo cha Watu wenye Ulemavu wa Jimbo la Shaurimoyo kilichojengwa
pembezoni mwa Skuli ya Sekondari ya Ufundi Mikunguni Mjini Zanzibar. Wa
kwanza kushoto ni Mkuu wa Mkoa Mjini Magharibi Mheshimiwa Ayoub Mohamed
Mahmoud.
Balozi
Seif akiangalia na kufurahia bidhaa zinazozalishwa na Watu wenye
Ulemavu wa Jimbo la Shaurimoyo ndani ya Kituo kipwa alichokizindua
rasmi.
Mjumbe
wa Kamati ya Mradi wa Kituo cha Watu wenye ulemavu cha Jimbo la
Shaurimoyo Bibi Mrashi Mikidadi akiwasilisha Risala kwenye hafla ya
uziduzi wa Kituo chao cha kazi za ujasiri amali pamoja na Ofisi.
Balozi
Seif akizungumza na Wananchi wa Jimbo la Shaurimoyo katika hafla ya
uziduzi wa Kituo chao cha kazi za ujasiri amali pamoja na Ofisi hapo
pembezoni mwa Skuli ya Sekondari ya Ufundi Mikunguni.
Balozi
Seif akimkabidhi Baskeli Mtoto mwenyeulemavu wa Jimbo la Shaurimoyo
Feisal Mbarouk kwenye hafla ya uziduzi wa Kituo chao cha kazi za ujasiri
amali pamoja na Ofisi hapo Mikunguni.
-
Mtoto Lutfia Mohamed ambae ni mlemavu akifurahia Baskeli mpya
aliyokabidhiwa na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali
Iddi zilizotolewa na Wafadhili mbali mbali.
Fundi
Seremala wa Kituo cha Watu wenye ulemavu cha Jimbo la Shaurimoyo Bwana
Juma Abdulaah Juma akipokea Baskeli yake itakayomsaidia katika harakati
zake za Kimaisha. Picha na – OMPR –ZNZ.
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...