Benki ya Biashara Mkombozi imezindua rasmi Tawi la Morogoro ambalo limepandishwa hadhi kutoka kituo cha huduma za kifedha na sasa kuwa tawi kamili.

Zoezi hili linafanyika wiki moja tu baada ya Benki ya Biashara Mkombozi kuzindua Tawi la Tegeta ambalo pia lilikuwa kituo cha cha huduma za kifedha hapo awali.

 Ufunguzi wa Tawi hilo ulifanywa na Katibu Tawala Wilaya ya Morogoro Bi. Ruth John akimwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Morogoro katika hafla iliyohudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Mkoa,  wadau mbalimbali, wafanyakazi, wafanyabiashara na wateja wa Benki ya Biashara Mkombozi.

 Akizindua tawi hilo jipya, mgeni rasmi aliipongeza Benki ya Biashara Mkombozi kwa hatua iliyofikia na kusema uzoefu kutoka nchi nyingine unaonyesha kuwa wafanya biashara wadogo na wale wakati ni wadau muhimu sana katika kukuza uchumi na kuondoa umasikini.

“Hivyo napenda kuwapongeza benki ya Biashara Mkombozi kwa kuamua kuwafikia wadau hawa muhimu ambao baadhi ya taasisi za kifedha zinawatizama kama ni soko hatarishi katika biashara ya kukopesha,” alisema.

Mgeni rasmi pia aliipongeza Benki ya Biashara Mkombozi kwa kutoa huduma za kibenki kwa watanzania wote bila ubaguzi wa rangi, ukabila, dini, dhehebu tofauti na baadhi ya watu wanavyotafsiri kuwa ni benki ya kanisa tu.

 “Natambua kuwa bado tuna changamoto kubwa ya kuwafikia na kuwashawishi watanzania walio wengi kutumia huduma za fedha za kibenki. Rai yangu kwenu Uongozi na Wafanyakazi wa Benki ya Biashara Mkombozi ni kwamba, mjikite zaidi katika ubunifu ili kuweza kuwavutia kundi hili ambalo linahitaji huduma zenu lakini labda utambuzi bayana bado haujakuwepo,” alisema.

Alitoa wito kwa Benki ya Mkombozi pia ijitahidi kufahamu mahitaji halisi ya soko na hivyo kuboresha huduma zake na bidhaa ili ziendane na mahitaji. “Elimu juu ya fedha kwa wananchi (yaani Financial literacy) ni muhimu sana, naomba pia muweke nguvu zenu katika hili,” alisema.
 Katibu Tawala wa Wilaya ya Morogoro, Ruth John  (wa tatu kulia) akikata utepe kuashiria uzinduzi wa Tawi jipya la Morogoro la Benki ya Biashara ya Mkombozi  huku viongozi na wageni waalikwa wakishuhudia tukio hilo.
Katibu Tawala wa Wilaya ya Morogoro, Ruth John akijaza fomu ya kufungua akaunti katika Benki ya Biashara ya Mkombozi baada ya kuzindua tawi jipya la Morogoro. 

Baadhi ya wafanyakazi wa benki ya Biashara ya Mkombozi Tawi la Morogoro wakifuatilia matukio ya uzinduzi wa tawi hilo.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...