FAMILIA ya Mohamed Dewj imetangaza dau ya shilingi  bilioni Moja kwa mtu atakayetoa taarifa ya kupatikana kwa bilionea huyo.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam mwanafamilia Azim Dewj amesema kuwa familia inashukukuru kwa ushirikiano walioupata kutoka serikalini kwa jitihada zinazoendelea za kumtafuta Mo Dewji.

Azim amesema taarifa zote zifike kwa Murtaza Dewji  kupitia namba za simu 0 755030014,0717208478, 0784783228 au kupitia barua pepe findmo@metl.net.

Amesema  familia inaahidi kwamba mtoa taarifa pamoja na taarifa zitaaki kuwa kubwa baina ya mtoa taarifa na familia.

Mtendaji Mkuu Wa Makampuni ya Metl Group Mohamed Dewji alipotea mnamo alfajiri ya saa 11:35 hadi 11:40 tarehe 11 Oktoba 2018 katika Hotel ya Collesseum Mtaa wa Haile Selasie Oysterbay Jijini Dar es Salaam. Familia kwa ujumla wanatoa shukrani serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na taasisi zake kwa jitihada kubwa wanazozifanya katika kuhakikisha kwamba motto wao anapatikana.

Pia wametoa shukurani kwa vyombo vya habari kwa kazi kubwa ya kuchukua jambo hili kwa uzito mkubwa na kuwataarifu umma, mbali na hilo taasisi za kidini na zisizo za kidini na kila mmoja wenu kwa maombi na kuwafariji katika kipindi hiki kigumu familia inachopitia.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...