HATIMAYE
Canada imeandika historia baada ya kuwa nchi ya pili duniani baada ya
Uruguay kwa kuhalalisha rasmi matumizi ya bangi hadharani kama dawa na
starehe.
Jarida
la Times nchini humo limeeleza kuwa baada ya miaka 95 ya kuzuiliwa kwa
matumizi ya bangi hatimaye Canada imetangaza rasmi matumizi ya bangi na
soko la kuuza bangi lilifunguliwa rasmi usiku wa kuamkia jumatano. Na
hiyo imekuja baada ya watu zaidi ya milioni 15 kutoa maoni yao katika
sanduku la posta na kupendekeza uhalalishaji wa matumizi ya bangi.
Imeelezwa
kuwa mwaka 2001 bangi iliruhusiwa kutumika kama dawa na hiyo ni baada
ya shinikizo kutoka kwa wabunge nchini humo na kwa sasa watatununua na
kutumia bangi hadharani bila bughudhi na polisi watahakikisha na
kukabiliana na visa vya uendeshaji magari wakiwa wamelewa bangi.
Uhalalishwaji huo umekuja baada ya ahadi ya waziri mkuu wa nchi hiyo
Justin Trudeau wa Liberal Party of Canada katika kampeni zake za mwaka
2015.
Na
baadhi ya wananchi wameonekana kununua bidhaa hiyo huku wakipewa risiti
ambazo zimekatwa kodi. Historia inaeleza kuwa mwaka 1923 matumizi ya
bangi yalipigwa marufuku nchini humo na kufikia mwaka 2001 bangi
iliruhusiwa kwa matumizi ya dawa pekee na Oktoba 17 mwaka huu bangi
imehalalishwa rasmi kwa matumizi ya dawa na starehe.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...