Na Humphrey Shao, Globu ya Jamii
ASKOFU  Mkuu Kanisa Katolini Jimbo Kuu la Dar es Salaam Mwadhama Polycap Cardinali Pengo ametoa salamu na ujumbe kwa Wakatoliki wote nchini kutumia muda huu wa kuadhimisha miaka 150 ya ujio wa kanisa  yatakayofanyika bagamoyo kwa kudumisha amani na unjilishaji hapa nchini.
Cardinal Pengo amesema tangu kuanzishwa kwa kanisa hilo hapa nchini Kanisa nchi yetu imetuwekea mazingira mazuri ya kuabudu na uhuru wa kuabudu nchini.
"Tunao uhuru wa kuabudu maana yake sio kanisa katoliki ndio libaki peke yake ibada zinafanyika kulingana na madhehebu na dini kama dini nyingine nchini na mashariki hatugombani licha ya kusikia watu wanamulekeo tofauti lakini bado atujasikia watu wakigombana kwa ajili ya dini"amesema Pengo.
Cardinal Pengo amesema kuwa katika miaka 150 ya Kanisa hapa Tanzania Bara Kanisa limeweza kutoa huduma za kijamii kwa kujenga Vituo vya Afya, Shule na huduma za Mawasiliano katika maeneo mbalimbali.

Pia amesema juu ya migogoro katika Makanisa na kusema kuwa migogoro katika Kanisa jambo linasikitisha haipaswi kuwepo kama watu wapo wanatafuta amani na wanamalengo kama ya Kanisa ni vyema ikakoma kabisa.
amemaliza kwa kusema kuwa katika kuhadhimisha miaka 150 ya Kanisa angetamani matokeo yake ni kuimarika kwa uinjilishaji na chimbuko lake jambo kuu lilete Mungano kwa wananchi wote licha ya kuwa na tofauti zetu za kidini na kiimani.
 Askofu Mkuu wa Jimbo Katoliki jimbo kuu la Dar es Salaam, Mwadhama Polycap Cardinali Pengo akizungumza na Waandishi wa Habari kuhusu Jubilei ya Miaka 150 ya kanisa Katoliki tangu liingie Tanzania bara na kusambaa mikoani.
Baadhi ya waandishi wa Habari wakifatilia Mkutano wa Askofu mkuu wa jimbo kuu la Dar es SalaamMwadhama Polycap Cardinali Pengo uliofanyika katika Kanisa la Mtakatifu Joseph Jijini Dar es Salaam leo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...