Na Tiganya Vincent
HALMASHAURI kuu ya CCM Mkoa wa Tabora imeipongeza Serikali ya Awamu ya tano kutokana na kutekeleza kwa vitendo Ilani yake ya miaka mitano tangu ulipofanyika uchaguzi Mkuu uliopita mwaka 2015 hadi sasa.

Pongezi hizo zimetolewa jana kwenye kikao maalumu cha wajumbe wa Halmashauri hiyo iliyokutana kupokea taarifa ya utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi kutoka serikali ya Mkoa wa Tabora.

Wajumbe hao walisema Serikali ya Awamu ya Tano chini ya Rais Dokta John Pombe Magufuli iliahidi miradi mbalimbali kwa wakazi wa Mkoa huo ikiwemo ya maji, afya, barabara na kilimo ambapo utekelezaji wake unaonekana kwa macho.

Waliitaja miradi ambayo utekelezaji wake umeanza na unaendelea kwa kasi mkoani humo kuwa ni wa maji kutoka ziwa Victoria kwa ajili ya wakazi wa Wilaya za Nzega, Tabora na Igunga.

Miradi mingine ni ujenzi wa barabara za kiwango cha lami kuunganisha Mkoa huo na mikoa jirani ambapo ujenzi unaendelea.

Katika hatua nyingine wajumbe hao wamezitaka Halmashauri  za wilaya mkoani humo kuhakikisha kiasi cha fedha inachotenga kutokana na mapato ya ndani kwa ajili ya vijana, akinamama, walemavu na ile ya miradi ya Maendeleo zinatumika kama ilivyokusudiwa.
  Katibu wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Tabora Janath  Kayanda akitoa maelezo ya awali kabla ya ufunguzi wa Kikao cha Halmashauri Kuu ya CCM Mkoa huo jana cha kupitia utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi.
 Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Tabora Hassan Wakasuvi akifungua Kikao maalumu cha Halmashauri Kuu ya CCM Mkoa huo jana cha kupitia utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi. 
 Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri ( wa pili kutoka kulia) akitoa taarifa ya utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi jana katika Kikao maalumu cha Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi  CCM Mkoa wa Tabora.
 Baadhi ya Wajumbe wa Hamashauri Kuu ya Cahama cha Mapinduzi Mkoa wa Tabora wakiwa katika kikao maalumu jana kupitia utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM. 
 Mbunge wa Urambo Margaret Sitta akiomba ufafanuzi jana wakati kikao maalumu jana Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Tabora cha kupitia utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM.
  Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kaliua Haruna Kasele akitoa maoni yake jana wakati kikao maalumu jana cha Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Tabora cha kupitia utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM. 
 Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Tabora-Uyui Saidi Ntahondi akitoa maoni yake jana wakati kikao maalumu jana cha Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Tabora cha kupitia utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM. Picha na Tiganya Vincent

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...