Imma Msumba, Arumeru.
Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Mh.Jerry Muro amefanya ziara ya kikazi ya kutembelea na kukagua Ujenzi wa Kituo cha Afya cha Mbuyuni kilichopo katika Halmashauri ya Arusha Dc  ambacho Serikali imetenga fedha Milioni 400 kwa ajili ya ujenzi wa Maabara na Nyumba ya Mtumishi wa kituo hicho pamoja na kufanya ukarabati wa majengo yaliyokuwepo kwa lengo la kuwapa wananchi huduma bora za afya na kupunguza vifo vitokanavyo na uzazi. 
 IMG-20181021-WA0010
IMG-20181021-WA0013
Dc Muro akikagua ujenzi wa Kituo hicho ameleza kuwa dhamira ya Serikali ya Awamu ya Tano ni kuleta mabadiliko makubwa katika sekta ya Afya kwa kuimarisha huduma za Afya na kujenga vituo vyenye hadhi vijijini.
 IMG-20181021-WA0006
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Bodi hiyo ya Ujenzi wa Kituo hicho Ndg.Leskara Olerangai Ambaye pia ni Diwani mstaafu wa kata ya Oljoro ameipongeza Serikali ya Awamu ya Tano chini ya Rais John Pombe Magufuli kwa  kuwezesha kutoa fedha kwa wakati huku akimpongeza Dc Muro kwa jitihada zake anazozifanya ili kuhakikisha ujenzi una kamilika kwa wakati.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...