Imma Msumba, Arumeru.
Mkuu wa Wilaya ya
Arumeru Mh.Jerry Muro amefanya ziara ya kikazi ya kutembelea na kukagua
Ujenzi wa Kituo cha Afya cha Mbuyuni kilichopo katika Halmashauri ya
Arusha Dc ambacho Serikali imetenga fedha Milioni 400 kwa ajili ya
ujenzi wa Maabara na Nyumba ya Mtumishi wa kituo hicho pamoja na kufanya
ukarabati wa majengo yaliyokuwepo kwa lengo la kuwapa wananchi huduma
bora za afya na kupunguza vifo vitokanavyo na uzazi.
Dc Muro akikagua
ujenzi wa Kituo hicho ameleza kuwa dhamira ya Serikali ya Awamu ya Tano
ni kuleta mabadiliko makubwa katika sekta ya Afya kwa kuimarisha huduma
za Afya na kujenga vituo vyenye hadhi vijijini.
Kwa upande wake
Mwenyekiti wa Bodi hiyo ya Ujenzi wa Kituo hicho Ndg.Leskara Olerangai
Ambaye pia ni Diwani mstaafu wa kata ya Oljoro ameipongeza Serikali ya
Awamu ya Tano chini ya Rais John Pombe Magufuli kwa kuwezesha kutoa
fedha kwa wakati huku akimpongeza Dc Muro kwa jitihada zake anazozifanya
ili kuhakikisha ujenzi una kamilika kwa wakati.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...