Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Bw. Charles Kichere akizungumza leo na watumishi wa Idara ya Huduma na Elimu kwa Mlipakodi waliopo TRA Makao Makuu jijini Dar es Salaam juu ya uboreshaji wa huduma mbalimbali za walipakodi.
Meneja wa Huduma na Elimu kwa Mlipakodi Bw. Gabriel Mwangosi (katikati) akitoa maoni wakati wa kikao na Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Bw. Charles Kichere kilichofanyika leo TRA Makao Makuu jijini Dar es Salaam.
Naibu Mkurugenzi wa Idara ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano Bi. Agnes Kitwanga akifafanua jambo wakati wa kikao na Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Bw. Charles Kichere kilichofanyika leo TRA Makao Makuu jijini Dar es Salaam. (PICHA ZOTE NA
VERONICA KAZIMOTO).
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...