FAMILIA ya sheikh Mohammed Ramiya, imeiangukia serikali na wizara ya utalii kuangalia uwezekano wa kuweka sehemu ya kumbukumbu kati ya hayati sheikh Ramiya na Mwl.J.K Nyerere, eneo la Zawiyani kata ya Dunda,Bagamoyo ili kuenzi historia ya ukombozi wa nchi yetu .

Aidha familia hiyo inakumbuka wakati marehemu sheikh Ramiya (78) akiugua kabla ya kufikwa na umauti wake mwaka 1985 ,Mwl. Nyerere alimchukua kumuuguza nyumbani kwake Msasani jijini Dar es salaam .

Akizungumzia namna anavyomkumbuka hayati Mwl.Nyerere, wilayani Bagamoyo mkoani Pwani, mtoto wa mwisho wa sheikh Ramiya, aitwae Ramiya Mohammed Ramiya alisema ,watalii wengi wakienda kwenye makumbusho za Bagamoyo wanakuta historia ya sheikh huyo na hayati Mwl. J.K Nyerere .

Alieleza watalii hao, huwa na shauku ya kwenda kujua historia ya picha na nyumba aliyokuwa akienda kufanyiwa dua muasisi huyo ,kisha kubarikiwa kwenda kuikomboa nchi mwaka 1961.

Ramiya alisema ,enzi hizo mwalimu Nyerere alikuwa rafiki wa sheikh Ramiya ,na alipelekwa huko na wazee wa Dar es salaam kwa nia ya kuombewa dua kwa ajili ya kupata uhuru bila kumwaga damu .

"Tukiacha marehemu baba kupigania uhuru,kuheshimika lakini pia sheikh Ramiya alikuwa mtu wa dini hivyo tutapendezwa kama serikali itatambua umuhimu wa kuweka makumbusho hiyo hapa basi iwe ya kidini zaidi " 

"Historia itakuwa haipotei ,lakini iwe tofauti kwa kuwa ni sehemu ya dini ,haitowezekana eneo hilo watu wakawa nje ya maadhi ya kiislamu ,isiruhusiwe wadada kwenda vichwa wazi ,ama kuvaa suruali bila kujistili " alibainisha Ramiya .
 Mtoto wa mwisho wa sheikh Ramiya ,aitwae Ramiya Mohammed Ramiya akielezea namna anavyomkumbuka hayati Mwl. J. K .Nyerere huko Zawiyani ,Bagamoyo. (Picha na Mwamvua Mwinyi)
 Mtoto wa mwisho wa sheikh Ramiya   ,aitwae Ramiya Mohammed Ramiya (wa kulia )akionyesha historia ya  nyumba aliyokuwa akienda kufanyiwa dua muasisi hayati Mwl.J.K Nyerere ,kisha kubarikiwa kwenda kuikomboa nchi mwaka 1961, nyumba ambayo kwasasa ina karne mbili  , imekuwa gofu na ilijengwa kwa mawe ,(wa kushoto) ,Mwenyekiti wa CCM Bagamoyo alhaj Abdul Sharif .
 Jumba lenye historia aliyokuwa akienda kufanyiwa dua muasisi hayati Mwl.J.K Nyerere ,kisha kubarikiwa kwenda kuikomboa nchi mwaka 1961, nyumba ambayo kwasasa ina karne mbili  , imekuwa gofu na ilijengwa kwa mawe ,ipo eneo la Zawiyani ,Dunda wilayani Bagamoyo.
Mtoto wa mwisho wa sheikh Ramiya, aitwae Ramiya Mohammed Ramiya, akionyesha historia ya picha mbalimbali baina ya hayati sheikh Ramiya na Mwl. J.K. Nyerere.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...