Na Humphrey
Shao, Globu ya Jamii
Naibu
Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, Mohamed Ali Ahmed ametaka kutungwa kwa sharia
Maalum kwa watu watakaobeza Muungano kutajwa kuwa ni wahaini.
Ahmed
Amesema hay oleo jijini Dar es Salaam wakati alipokuwa akichangia Mada katika
kongamano la Kumbukizi ya Mwalimu Nyerere lililobebwa na Mada ya ‘Falsafa ya
Mwalimu Nyerere juu ya Kujitegemea na Maendeleo ya Viwanda Tanzania’.
“mimi
ninachoomba tuvutane tu ila tuwandalie mstakabali mzuri hao wanakuja nyuma yetu
na tuwajenge hawa kwa mazuri nimeguswa kidogo na katibu wa baba wa Taifa pale
alipouliza nyie vipi huko katika vyama vya siasa nimekuwa nashangaa sana
wanasiasa awajui kupambanua kipi cha kubeza na kipi sio cha kubeza”
Ahmed
amesema kuwa kuna tatizo la kisheria katika mfumo wa kuongoza hivi vyama kwani
wanasiasa ndio wamekuwa kipaumbele kuhoji muungano jambo ambalo linafanywa kwa
utashi wa kulenga kupata kura tu.
Amesema ifike
wakati wakusema kuwa mtu akigusa Muungano ni uhaini sio kwa kumgusa Rais Peke
yake kwani wanfanya hivi kwa kutaka kupata umaharufu wa kisiasa.
Amesema ifike
mahali ni sharia kufata fikra za Mwalimu kwani anayekiuka hizo atakuwa ametenda
kosa kubwa la jinai kwani tukiacha uhuru tutaendelea kudanganyana siku hadi
siku.
Alimaliza kwa
kusema kuwa leo amekuja Rais Dk John Magufuli anasimamia haya lakini ipo siku
atakuja kiongozi atayaaopuuza haya anayofanya kisha taifa hili litapromoka kwa
kiwango cha ajabu nakupoteza nguvu yote hii.
Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Prof. Faustine Kamuzora akitoa mada ya Umuhimu wa Taifa huru na uhuru wa Wananchi katika kukuza uchumi wa Viwanda.
Mkuu wa Wilaya ya Kigambboni Sarah Msafiri akizungumza kuhitimishaKongamano la Kumbukizi ya Mwalimu Nyerere.
Picha ya Washiriki wa Kongamano la Kumbukizi ya Mwalimu Nyerere Lililofanyika katika Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere Kampasi ya Kivukoni Dar es Salaam.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...