UTAFITI wa kutathmini upatikanaji wa Huduma za Uzazi wa Mpango pamoja na dawa zinazohusiana na huduma za uzazi nchini utanarajiwa kufanyika mwishoni mwa mwezi Oktoba waka huu.

Akifungua mafunzo ya siku kumi na moja kwa wadadisi wa utafiti huo, Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) Dk. Albina Chuwa amesema taarifa zitakazokusanywa kwenye utafiti huo ni pamoja na upatikanaji wa njia za uzazi wa mpango katika ngazi mbalimbali za vituo vya kutolea huduma za afya.

Aidha, kwa mujibu wa Mkurugenzi Mkuu huyo, utafiti huo utakusanya taarifa zinazohusu mfumo wa ugavi wa dawa au vifaa vinavyohusiana na njia za uzazi wa mpango pamoja na huduma za uzazi na uwepo wa watumishi waliosomea utoaji wa huduma hizo.

Utafiti huo ambao ni mara ya tatu kufanyika nchini kuanzia mwaka 2015 utaangalia pia uwepo wa miongozo mbalimbali kutoka wizara za afya inayoongoza huduma hizo na pia utakusanya maoni ya wateja waliofika kwenye kituo husika kwa ajili ya huduma za uzazi wa mpango.
Mkurugenzi wa Shughuli za Kitakwimu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) Irenius Ruyobya akizungumza leo mkoani Morogoro kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa NBS, Dkt. Albina Chuwa wakati wa ufunguzi wa Semina ya mafunzo ya wadadisi wa Utafiti wa kutathmini upatikanaji wa Huduma za Uzazi wa Mpango.
Baadhi ya wadadisi wa utafiti wa kutathmini upatikanaji wa Huduma za Uzazi wa Mpango ambao ni wauguzi na madaktari kutoka katika Hospitali na Zahanati mbalimbali nchini wakifuatilia hotuba ya mgeni rasmi (hayupo pichani) wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo yanayoendelea mkoani Morogoro.
Baadhi ya wadadisi wa utafiti wa kutathmini upatikanaji wa Huduma za Uzazi wa Mpango ambao ni wauguzi na madaktari kutoka katika Hospitali na Zahanati mbalimbali nchini wakifuatilia hotuba ya mgeni rasmi (hayupo pichani) wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo yanayoendelea mkoani Morogoro. 


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...