Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
KATIKA harakati za kutaka kuokoa nguvu kazi ya vijana walioathirika na madawa ya kulevya Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kuchumi (NEEC) limepanga kuandaa program kabambe ya kuwawezesha kwa waliokubali kuachana na matumizi ya madawa hayo baada ya kupata tiba kutoka vituo vya tiba ili wakazalishe mali.

Mwenyekiti wa baraza hilo Dkt. Festus Limbu amesema hayo jijini Dar es Salaam mwishoni mwa juma wakati wa kikao na vijana waliokuwa wanatumia dawa hizo na ambao wanapata tiba katika vituo vya Hospitali ya Muhimbili, Temeke na Mwananyamala, kuwa baraza limejipanga kuwaletea program ya uwezeshaji ili waweze kujiletea maendeleo.

“Baraza limejipanga kuokoa kundi lenu hasa kwa wale waliokubali kuachana matumizi ya madawa ya kulevya na waopata tiba katika vituo mbalimbali nchini,” uwezeshaji unaolengwa ni wa kupata ardhi, mafunzo, mitaji na masoko, aliongeza kusema, Dkt Limbu.

Alisema uwezeshaji huo utawafikia baada ya kuwachambua kulingana na shughuli wanazoweza kufanya kupitia vikundi ambavyo vitaundwa ili kutoa fursa ya kuwawezesha kwa karibu zaidi.
 Mwenyekiti wa Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC),Dkt. Festus Limbu wa pili kushoto akisistiza jambo wakati alipokuwa akizungumza na vijana wanaopata tiba ya kuachana na matumizi ya madawa ya kulevya wa Vituo vya Hospitali ya Muhimbili, Temeke na Mwanyanyamala, wa tatu kulia ni Katibu Mtendaji wa baraza hilo, Bi. Beng’I Issa, wa pili kulia ni Mjumbe wa baraza hilo, Bi. Dkt. Astronaut Bagile, kushoto Kamishina wa Kinga na Tiba Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Madawa ya Kulevya na kulia afisa toka baraza hilo, Bw. Jozaka Bukuku.
Mwenyekiti wa Baraza la Taifa la Uwezeshaji wananchi Kiuchumi (NEEC),Dkt.Festus Limbu kushoto akifafanua jambo wakati alipokuwa akizungumza na vijana wanaopata tiba ya kuachana na matumizi ya madawa ya kulevya katika Vituo vya Hospitali ya Muhimbili, Temeke na Mwananyamala wengine ni vijana hao.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...