*Waziri Mkuu aagizwa achukuliwe hatua

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amemuagiza Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kagera, Augustine Ollomi awachukulie hatua askari polisi wote wa wilaya ya Kyerwa wanaotuhumiwa kusindikiza kahawa ya magendo inayouzwa nchi jirani akiwemo Mkuu wa Polisi wa Wilaya hiyo, Justin Joseph.

Ametoa agizo hilo leo (Jumapili, Oktoba 7, 2018) baada ya kukagua kiwanda cha kukoboa kahawa cha Nkwenda wilaya Kyerwa katika siku ya pili ya ziara yake ya kikazi mkoani Kagera. Katika ziara hiyo Waziri Mkuu ameambatana na Mkewe Mama Mary Majaliwa.

“Askari polisi wa wilaya ya Kyerwa pamoja na OCD wao wanatuhumiwa kusindikiza kahawa inayosafirishwa kwa njia ya magendo kwenda nchi ya jirani kupitia njia mbalimbali zisizo rasmi zikiwemo za Kumisongo, Kashaijo na Omukatoma.”

Waziri Mkuu amesema ni jambo la hatari kama askari Polisi wanasindikiza kahawa inayouzwa kwa magendo, hivyo ameagiza jambo hilo lidhibitiwe haraka.”Marufuku kupeleka kahawa nje ya nchi kwa njia ya magendo na polisi msishiriki katika butura.”

Katika hatua nyingine,Waziri Mkuu amesema kuanzia msimu ujao wa kahawa, minada yote ya kahawa inayozalishwa mkoani Kagera itafanyika ndani ya mkoa huo badala ya kufanyika Moshi, mkoani Kilimanjaro.
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizindua Kiwanda cha Kukoboa Kahawa cha Kaderes kilichopo eneo la Nyakatuntu wilayani Karagwe Oktoba 7, 2018.  Kulia ni Mkewe Mary na kushoto ni Mkurugenzi  wa kiwanda, Leonard Kachobonaho. Wapili kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Brigedia Jenerali Marco  Elisha Gaguti. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
  Waziri Mkuui, Kassim Majaliwa na mkewe Mary (kulia) wakimfariji mtoto , Mathews Martin aliyelazwa katika Kituo cha Afya cha Kayanga wilayani Karagwe, Oktoba 7, 2018. Kushoto ni Mama wa mtoto huyo, Joyce Martin.

 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akimwagilia mti alioupanda baada ya kutembelea Kituo cha Afya cha Kayanga kilichopo Karagwe, Oktoba 7, 2018. Wapili kulia ni mkewe Mary.
  Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na Mkewe Mary wakiwapungia wananchi wakati walipowasili kwenye uwanja wa Kayanga Changarawe, Karagwe kuhukutubia mkutano wa hadhara, Oktoba 7, 2018.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...