Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Zainab Telack akiliangalia gari alilokabidhiwa kwa ajili ya Jeshi la Polisi wilayani Kishapu.

Na Robert Hokororo, Kishapu

Jeshi la Polisi Wilaya ya Kishapu mkoani Shinyanga limepokea gari jipya kwa ajili ya matumizi ya shughuli zake kutoka mgodi wa almasi wa Mwadui.

Gari hilo aina ya Nissan Hilux lenye thamani ya sh. milioni 80 limepokelewa na Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Zainab Telack ambaye alikabidhi jeshi hilo.

Akizungumza katika hafla ya makabidhiano ya gari hilo yaliyofanyika wilayani humo Mhe.Telack aliushukuru mgodi kwa msaada huo. Telack ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama Mkoa alisema kuwa gari litawezesha shughuli za Polisi kufanyikaa kwa ufanisi.

Aliwaomba wasichoke kuendelea kuisaidia Kishapu pamoja na kushirikiana na Serikali ya wilaya hiyo kwani wao pia ni sehemu ya jamii hiyo.

Aidha alilitaka jeshi hilo kulitumia gari hilo walilokabidhiwa kwa matumzi yaliyokusudiwa ya kulinda wananchi ili waendelee kuwa na imani nalo.
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Zainab Telack akitoa maelekezo na kumkabidhi funguo na kadi ya gari Mkuu wa Polisi Wilaya (OCD) ya Kishapu, Emmanuel Galiyamoshi. Anayeshuhudia kushoto ni Alchelaus Mutalemwa.
Sehemu ya maafisa wa Jeshi la Polisi wilayani Kishapu wakinyakua baada ya kushuhudia makabidhiano ya gari.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...