Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Zainab Telack akiliangalia gari alilokabidhiwa kwa ajili ya Jeshi la Polisi wilayani Kishapu.
Na Robert Hokororo, Kishapu
Jeshi la Polisi Wilaya ya Kishapu mkoani Shinyanga limepokea gari
jipya kwa ajili ya matumizi ya shughuli zake kutoka mgodi wa almasi
wa Mwadui.
Gari hilo aina ya Nissan Hilux lenye thamani ya sh. milioni 80
limepokelewa na Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Zainab Telack
ambaye alikabidhi jeshi hilo.
Akizungumza katika hafla ya makabidhiano ya gari hilo yaliyofanyika
wilayani humo Mhe.Telack aliushukuru mgodi kwa msaada huo.
Telack ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama
Mkoa alisema kuwa gari litawezesha shughuli za Polisi kufanyikaa
kwa ufanisi.
Aliwaomba wasichoke kuendelea kuisaidia Kishapu pamoja na
kushirikiana na Serikali ya wilaya hiyo kwani wao pia ni sehemu ya
jamii hiyo.
Aidha alilitaka jeshi hilo kulitumia gari hilo walilokabidhiwa kwa
matumzi yaliyokusudiwa ya kulinda wananchi ili waendelee kuwa na
imani nalo.
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Zainab Telack akitoa maelekezo
na kumkabidhi funguo na kadi ya gari Mkuu wa Polisi Wilaya (OCD)
ya Kishapu, Emmanuel Galiyamoshi. Anayeshuhudia kushoto ni
Alchelaus Mutalemwa.
Sehemu ya maafisa wa Jeshi la Polisi wilayani Kishapu wakinyakua
baada ya kushuhudia makabidhiano ya gari.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...