Waziri wa Maji, Profesa Makame Mbarawa amekerwa na wakandarasi wababaishaji ambao wamekuwa wakichangia miradi mingi ya maji kuchelewa kukamilika au kujenga miradi yenye viwango duni na kuisababishia Serikali matatizo na wananchi wake.

Hali hiyo imetokana na kukosekana kwa mkandarasi katika eneo la kazi kwenye mradi wa Nanyamba-Mlanje, katika Wilaya ya Nanyamba mkoani Mtwara wakati alipofika kukagua mradi, kitendo ambacho hakukifurahia.

Profesa Mbarawa amesema alitegemea kumkuta mkandarasi huyo site ili aweze kuzisikia changamoto zinazomkabili na kuzipatia ufumbuzi ili mradi huo uweze kukamilika mara moja na kutoa huduma.Akiongea na wakazi wa Mlanje, Profesa Mbarawa amesema ametoka kuidhinisha malipo ya Shilingi Milioni 93 kwa mkandarasi huyo wiki iliyopita lakini ameshangazwa na kutomkuta akifanya kazi, na kuwaambia wakandarasi wasiokaa site ni wababaishaji na hawafai.

“Wakandarasi wa namna hii ni wababaishaji hawatufai na siwataki kwa sababu wanaigombanisha Serikali na wananchi, wakikwamisha mipango ya Serikali na wananchi wakiendelea kukosa maji bila sababu za msingi. Sitaki wakandarasi wa aina hii na ndio maana tumewafukuza waliokuwa kwenye miradi ya Kigoma na Lindi kutokana na tabia za ubabaishaji’’, amesema Profesa Mbarawa.
Mhandisi wa Maji Wilaya ya Nanyamba, Moses Msuya akimuonyesha Waziri wa Maji, Profesa Makame Mbarawa mpango ya utekelezaji wa mradi wa Nanyamba-Mlanje.
Waziri wa Maji, Profesa Makame Mbarawa akikagua matenki ya mradi wa Nanyamba-Mlanje katika Wilaya ya Nanyamba, mkoani Mtwara.
Waziri wa Maji, Profesa Makame Mbarawa akiwa kwenye mradi wa Mkwiti, katika wilaya Tandahimba, mkoani Mtwara.
Waziri wa Maji, Profesa Makame Mbarawa akisalimiana na baadhi ya viongozi wa Wilaya ya Newala, akiongozwa na Mkuu wa Wilaya, Aziza Mangosongo.
Waziri wa Maji, Profesa Makame Mbarawa akisikiliza taarifa inayosomwa na Mhandisi wa Maji Wilaya, Nsajigwa Sadiki. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...