Waziri wa Maji, Profesa Makame Mbarawa  amezindua rasmi Kampeni ya Upandaji Miti kandokando ya vyanzo vya maji nchi nzima mkoani Mtwara kwa lengo la kuhakikisha vyanzo hivyo vinatunzwa na kuwa endelevu kwa miaka mingi ijayo.
Profesa Mbarawa amezindua kampeni hiyo kwa kupanda miti nane katika chanzo cha Mtawanya kilichopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Mtwara Mjini na kuzitaka Bodi zote za Mabonde tisa nchini kuweka mkazo na mipango madhubuti ya kusimamia na kutunza rasilimali za maji ziweze kuwa endelevu.
Ametoa agizo hilo kutokana na uvamizi na uharibifu mkubwa wa vyanzo vya maji katika maeneo mengi kwa sasa nchini, hali inayohatarisha kiasi kikubwa cha maji kupungua kutokana na vyanzo vingi kukauka, hali inayoweza  kusababisha ukosefu wa maji ya kutosha kwa ajili ya miradi inayoendelea kutekelezwa na Serikali.
Na kutaka vyanzo vyote vya maji vitunzwe na kulindwa kwa kupandwa miti maalumu inayohifadhi maji na kuagiza wale wote wanaofanya shughuli za kibinadamu kwenye vyanzo waache tabia hiyo na watakao kaidi wachukuliwe hatua kali ili iwe fundisho kwa wengine kwa kuwa sheria inaweka bayana kuhusu jambo hilo. 
Ametoa tamko hilo kwa kuzingatia Sheria ya Maji Na, 11 ya Mwaka 2009 inayokataza kufanya shughuli za kibinadamu katika vyanzo vya maji, na ikieleza shughuli zote za kibinadamu zifanyike umbali wa mita 6o kutoka chanzo cha maji kilipo na kutaka maeneo yote yawekewe mipaka na vizuizi kuonyesha ukomo wa watu kuingia kwenye vyanzo hivyo.
 Waziri wa Maji, Profesa Makame Mbarawa akiwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mzingira Mtwara (MTUWASA), Mhandisi Mashaka Sita katika Mitambo ya Maji Mangamba, Mtwara MJini.
 Waziri wa Maji, Profesa Makame Mbarawa akizungumza na wakazi wa Msanga Mkuu, Mtwara Vijijini.
Waziri wa Maji, Profesa Makame Mbarawa akiinama kwa ajili ya kuonja na kujua ubora wa maji katika mradi wa Mpapura, Mtwara Vijijini.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...