Na.Vero Ignatus ,Arusha

Kila mwaka mkoa unatakiwa kutenga fungu kwaajili ya kuandaa tamasha la urithi na utamaduni itakayochangia kuzaa zao jipya la utalii na kupanua wigo wa vivutio vya utalii nchini.

Hayo yamesemwa na Katibu mkuu wizara ya Habari Utamaduni na Michezo Suzan Mlawi katika uzinduzi wa Tamasha la Urithi lililozinduliwa Jijini Arusha katika uwanja wa Shekh Amri Abeid na kushirikisha makabila mbalimbali mkoani hapo.Ameeleza kuwa Taifa lisilo na utamaduni ni taifa lililokufa, sambamba na kupoteza rasilimaliza husika kwani utamaduni ni kuvutio kibwa cha utalii.

"Tusipoenzi na kuzitunza tamaduni hizo utu wetu rasilimali zetu zitapotea, kwani utamaduni wetu ni kivutio kikubwa cha utalii"alisema Katibu Suzan Kwa upande wake Katibu tawala wa Mkoa wa Arusha Richard Kwitega amesema asilima 80%wageni wanaoingia nchini wanatembelea Mkoani hapo kutokana na vivutio vilivyopo mkoani Arusha kupitia vya utalii Maonyesho hayo yamehusisha wadau kuonyesha mambo burudani,ngoma za asili,vyakula vya asili,mavazi ya asili ,utalii na tamaduni za Mtanzania bila kuvunja sheria .

Katibu mkuu Wizara ya Habari Utamaduni na Michezo Suzan Mlawi akizungumza na wananchi wa Mkoa wa Arusha katika Tamasha la Urithi Festival lililozinduliwa mkoani Arusha. Picha na Vero Ignatus
Katibu mkuu Wizara ya Habari Utamaduni na Michezo Suzan Mlawi akiwa katika moja ya banda wanalotengeneza vitu vya asili. Picha na Vero Ignatus. 
Kutoka katikati ni Katibu mkuu wizara ya Habari Utamaduni na Michezo Suzan Mlawi, kulia kwake ni Mkurugenzi mkuu wa Makumbusho ya Taif a Profesa Audix Mabula ambaye pia ni Mwenyekiti wa maandalizi ya Tamasha la Urithi, akifuatiwa na Katibu tawala wa Mkoa wa Arusha Richard Kwitega.
Hawa nao wakinamama kutoka kabila la Kimaasai walipamba Tamasha hilo la Urithi na utamaduni mkoani Arusha katika uwanja wa Shekh Amri Abeid. Picha na Vero Ignatus.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...